HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

December 28, 2014

NICKK WA PILI:MSANII NYOTA WA HIP HOP NCHINI,NI MWANAMUZIKI MSOMI,AMESHIRIKI KATIKA FURSA MBALIMBALI ZA KIJAMII NA KUTOA HITS SONGS KIBAO NA ANAMKUBALI ZAIDI JOH MAKINI NA JAY Z


Akizungumza katika moja ya fursa ya kijamii  nchini

MAFANIKIO siku zote huanza kujengwa na fikra zilizo imara ndicho kitu kinachomfanya Msanii wa muziki wa Hip Hop nchini kutoka katika kundi la weusi,Nickson Saimoni maarufu kama 'Nickk Wa Pili' kuzidi kuwa nyota inayong'ara kwa wasanii wengine nchini.

Kama ilivyowazi kuwa msanii huyu ni msomi ambaye amefanikiwa kushiriki katika fursa mbalimbali za kijamii ambazo anaamini zimechangia kumkuza zaidi kiakili na kutambua uhalisia wa maisha ya mtanzania kuliko alivyosoma darasani.
Baada ya kumaliza elimu ya shahada katika chuo kikuu cha Dar es salaam
                    Historia yake
Nickk wa pili alizaliwa katika hospitali ya Maunt Meru mjini Arusha na kuoma elimu ya sekondari katika shule ya sekondari Arusha kidato cha kwanza mpaka cha nne na kumlizia Kigoma kidato cha tano na sita na kujiunga elimu ya juu katika chuo kikuu cha Dar es salaam mwaka 2007.

Alipenda na akijua kuimba muziki tangu akiwa elimu ya sekondari na kupata umaarufu akiwa mwaka wa pili chuo kikuu cha Dar es salaam mwaka 2008 baada ya kushirikishwa katika wimbo wa Joh makini ujulikanao kama 'Niaje Nivipi'.
Bada ya kujulikana alianza kutambulisha kazi zake zikiwemo Good Boy aliyofanya na Msanii maarufu wa Rnb nchini Rama D na wimbo ujulikanao kama 'Higher' aliofanya mwandaaji Pancho Latino na alimshirikisha Joh makini.

Hakuishi hapo aliendelea kufanya vibao vingine vingi vikiwemo 'Bum Kubam'  aliyomshirikisha G-Nako, Sitaki kazi aliyomshirikisha Ben Pol na Joh Makini bila kumsahau G-Nako.

Kazi zingine alizofanya ni kitu changu kizuri aliyomshirikisha Lina,hatuendani aliyomshirikisha Belle 9 na Kiujamaa aliyomshirikisha Pipi.
Akiwa na kundi lake la weusi
Anauchukuliaje uwezo wa msanii G-Nako kutokana na kumshirikisha nyimbo nyingi.
Nikk Wa Pili alisema kuwa G-Nako ni msanii mwaenye ufundi na uwezo wa hali ya juu na mara nyingi huwa wanakuwepo pamoja studio anaporekodi ndoyo maana mara nyingi wanafanya kazi pamoja.

Kama ilivyo wazi ni kwamba wasanii hawa mbali na kuwa kundi moja pia wamefanya kazi kadhaa kwa kushirikiana zikiwemo 'Pea',Bum Kubam,sitaki kazi,Mavijana.

Mtazamo wake kwa kundi la muziki la weusi
Kundi hili lililoundwa na wasanii walikuwa katika makundi ya River Camp Soldier na Nako 2 Nacko ,linaundwa na wasanii watano ambao ni, G-Nako,Joh Makini,Bonta,Lord Eyes na yeye mwenyewe Nick Wa Pili.

Nick Wa Pili anasema kuwa kampu ni weusi ipo kwa ajili ya kutengeneza muziki mzuri nchini na tayari hatua zinafanyika na washabiki wa muziki wao wanafurahia.

Alimtaja msanii ambaye ni kioo na mwongozo wake nchini na nje.
Nick Wa Pili hakusita kumtaja msanii maarufu wa Hip Hop nchini,Joh Makini kuwa ni taa na mongozo wa muziki wake.

"Joh Makini ni msanii mkongwe mwenye uwezo wa ajabu na wa juu sana katika wasanii nchini".Alisema Nickk Wa Pili.

Aliongeza kuwa kwa upande wa nje anamkubali msanii wa mashuhuli duniani ajulikanaye kama 'Jaz Z'.
Alifunguka kuhusu producer Nah reel
"Nah Reel ni mwandaaji maarufu wa muziki anayejua kwenda na wakati anafanya muziki unaopendwa na mashabiki kila kukicha".Alisema
Aliongeza kuwa licha ya muandaaji huyo kuwa mtu wa karibu(rafiki) lakini anaamini kila mtu anaujua vizuri uwezo wa mwandaaji huyo ambaye alifanya naye kazi akiwa studio za Kama kawa Record,Home Town Record na sasa katika The Industry ambako kote alifanya kazi zilizopenda na mashabiki wa muziki wake.

Akizungumzia programu ya fursa ya Clouds Media
Nickk Wa Pili alisema kuwa programu hiyo ilimfanya kufanya utafiti wa maisha halisi ya mtanzania kitu ambacho hata darasani hakufundishwa.

Nickk Wa Pili alieleza kuwa programu hiyo ilikuwa na lengo la kuhamasisha vijana na kupata ushuhuda wa kujifunza kutoka kwa watu waliofanikiwa iliyokuwa safari ya kuzunguka mikoa yote nchini.

                       Matatizo/changamoto
Nick wa Pili anasema kuwa muziki wetu unachangamoto kubwa kwani katika vyombo vyetu vya habari nchini unachezwa muziki usio na viwango hali inayofanya muziki mzuri nchini kutopewa thamani na kuonekana mbaya.
Ineandaliwa na Sylvester David

Email:muzikibegani@gmail.com

Call:0715577805 au 0768538085

No comments:

Post a Comment

Pages