HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

May 17, 2015

CUF KIGOGO WAANZA MCHAKATO WA KUMPATA MGOMBEA

CHAMA cha Wananchi (CUF), Kata ya Kigogo wilayani Ilala Dar es salaam kimepiga kura ya maoni kwa ajili ya kupata mgombea atakayeweza kupambanishwa na wagombea wengine Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).

Vyama vinavyo unda umoja huo ni Chama cha Wananchi (CUF), Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), NLD na NCCR-Mageuzi.

Akizungumza na wandishi wa habari kuhusu mchakato huo, Katibu Kata wa CUF Kata ya Kigogo, Khalid Singano ambaye pia ni mgombea wa chama hicho, alisema wanachofanya ni hatua ya awali.

Alisema baada ya kura hiyo ya ndani mshindi atashindanishwa na wagombea wengine kutoaka vyama vinavyounda umoja huo kwa ajili ya kumpata mshindi wa jumla atakayepambana na yule Chama Cha Mapinduzi (CCM).

“Vigezo vitakavyotumika kumpata mshindi huyo wa jumla, itaangaliwa takwimu za vyama vyote zinazohusiana na chaguzi mbalimbali zilizopita, kukubalika kwa chama na kukubalika kwa mgombea,”alisema Singano.

Singano, aliwataja wagombea hao kuwa ni Mwinyi  Madenge, Baraka Nyakite, Iddi Maza, Sellemani Sellemani pamoja na yeye mwenyewe (Singano).

Alisema upepo wa kura hizo za ndani ulikuwa ukiangalia zaidi uwezo wa watendaji ambao wameweza kukisaidia chama na kukifanya kipate mitaa mitatu katika uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka jana.

“Sio dhambi mimi ni miongoni mwa watendaji wa chama hiki tuliyoshiriki katika kukiimarisha katika kata hii ya kigogo kwa hiyo uwezo wa kuongoza kata ni nao,”alisema.


Hadi gazeti hili linakwenda mitamboni matokeo yalikuwa bado hayajatangazwa.

No comments:

Post a Comment

Pages