HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 24, 2017

DG WA PPF WILLIAM ERIO AUNGANA NA WAFANYAAKZI KUHUDUMIA WATEJA, NI KWENYE KILELE CHA WIKI YA UTUMISHI

 Mkurugenzi Mkuu wa PPF, Bw. William Erio, (kushoto), akismikiliza Mwanachama wa Mfuko huo, Bw.Clemence Munisi, aliyefika kitengo cha huduma kwa wateja ili kuhudumiwa wakati wa kilele cha wiki ya utumishi Makao Makuu ya PPF Barabara za Samora/Morogoro jijini Dar es Salaam, Ijumaa Juni 23, 2017.


NA K-VIS BLOG/Khalfan Said

WAKATI siku ya Wiki ya Utumishi wa Umma imefikia kilele leo Juni 23, 2017, Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Bw. William Erio, aliiacha ofisi yake na kujiunga na kitengo cha Huduma kwa Wateja cha Mfuko huo Makao Makuu ya PPF barabara ya Samora na Morogoro jijini Dar es Salaam ambapo alifanya kazi ya kuwahudumia wateja.

Awali Bw. Erio alizungumza na baadhi ya wanachama wa Mfuko waliofika kwenye kitengo hicho kuhudumiwa, na kusikiliza maoni yao ni jinsi gani wanahudumiwa na Wafanyakazi wa Kitengo hicho. 

Idha Mkurugenzi Mkuu Erio pia aliwahudumia wanachama wengine akiwemo mzee Clemence Munisi ambaye ni mstaafu wa kampuni ya Narco.

Kwa mujibu wa Mzee Munisi, yeye alisema, amefurahishwa na huduma zitolewazo na Mfuko ambapo zimekuwa ni za haraka na zisizokuwa na usumbufu.

Baada ya kutembelea kitengo hicho, Bw. Erio alikutana na baadhi ya wafanyakazi ili kusikiliza maoni yao kuhusu namna uongozi wa Mfuko unavyoshirikiana na wafanyakazi katika kulihudumia taifa.

“Kama mjuavyo hii ni siku ya mwisho ya wiki ya utumishi, nimeona nikutane nanyi ili kuwasikiliza, maana mara nyingi sisi viongozi ndio tunasema tu, lakini leo ni zamu yenu ninyi watumishi kusema jambo lolote linalohusu Shirika letu, lakini hata wewe binafsi kama mfanyakazi.” Alisema Bw. Erio.

Bw. Erio pia aliwakumbusha wafanyakazi kuwajibika ipasavyo katika kuwahudumia wananchi, lakini pia kuzingatia suala la afya bora.
“ Ili uweze kuwahudumia vema wananchi, ni lazima uwe na afya bora, mimi kama mwenyekiti wa kamati ya UKIMWI ya shirika letu, bado nasisitiza, chukueni tahadhari kubwa, kwani ugonjwa huu bado upo ingawa hauzungumzwi sana kwa sasa.” Alionya Bw. Erio.

Bw Erio pia aliwataka wafanyaakzi hao kutojihusisha kwa namna yoyote na matumizi ya madawa ya kulevya au biashara ya madawa ya kulevya.

Mimi siko serikalini, lakini ninao wajibu kama kiongozi wenu, kuwakumbusha mambo ambayo jamii inapaswa kujiepusha nayo, na nyinyi kama sehemu ya jamii, hamna budi kutojihusisha kwa namna yoyote na matumizi au biashara ya madawa ya kulevya.” Alisema.

Kwa upande wao wafanyakazi walishukuru uongozi wa Mfuko kwa kuwa karibu na wafanyakazi. “Ukiona hupati maneno mengi ujue mambo yako poa, sisi kwakweli tunashukuru sana kwa kiongozi kama wewe kuja kusungumza nasi tena kwa kutusikilzia sisi tuna lipi la ksuema, lakini nikuhakikishie tu kwa niaba ya vijana wenzangu, mimi naona mambo yako safi na sikukuu hii tutasherehekea kwa furaha kabisa.” Alisema mfanyakazi mmoja kutoma idara ya fedha, Bw.Joseph Fungo.

Naye Meneja wa fedha wa PPF, Bw.Dozitte Msoffe, yeye alisema, mahusiano mema kati ya uongozi na wafanyakazi ndiyo yanayoboresha utoaji huduma kwa wananchi na kwa PPF, kumekuwepo na mahusiano mazuri sana baina ya pande hizi mbili kwa hivyo mimi nikupongeze tu ndugu Mkurugenzi Mkuu, kwa uamjzi wako wa kuja kutusikiliza hii huwezi kuisikia mahala pengine, lakini hapa PPF imetokea hongera sana.” Alsiema Bw. Msoffe.
 Bw. Erio akizungumza na baadhi ya wanachama waliofika kitengo cha huduma kwa wateja cha Mfuko huo ili kupaiwa huduma
 Meneja wa Fedha wa PPF, Bw. Dozitte Msoffe akizungumza. Kulia ni Meneja Uhusiano wa Mfuko huo, Bi. Lulu Mengele.
 Baadhi ya wafanyakazi wakimsikiliza Bw. Erio.
 Bw. Msoffe akizungumza na Mkurugenzi Mkuu wa PPF, Bw. Erio na watumishi wengine wakimsikilizia
 Baadhi ya wafanyakazi wakimsikiliza Bw. Erio kwa makini
 Afisa Fedha wa PPF, Bw. Joseph Fungo akizungumza
 Baadhi ya wafanyakazi wakipiga makofi kufuatia mazungumzo mafupi ya Bw. Erio.
Kaimu Mkurugenzi wa Rasilimali Watu, Bi. Gladness Mteta, (kulia) akiwa na Meneja wa Huduma za Utawala wa PPF, Bi. Cecilia Obeid Katikaza.

No comments:

Post a Comment

Pages