NA KENNETH NGELESI, MBEYA
UKOSEFU wa elimu na Taarifa sahihi juu ya Mifuko na Mipango (Programu)ya
ewezeshaji na Taasisi na vikundi vya kifedha vya kijamii nchini ni moja ya
sababu zinizochangia kuwepo na maudhurio hafifu ya wananchi katika Moanesho ya
taasisi hizo yanayoendelea katika
Viwanja vya Shule ya Msingi Ruanda Nzovwe jijini Mbeya.
Hayo yamebainishwa na Mwakilishi ya Mpango wa kunusuru kaya
Maskini TASAF,Dismas Yusuph wakati wa
Majumuhisho ya Maonesho hayo huku akieleza kuwa elimu bado haijatolewa na
wananchi hawana taarifa sahihi juu ya mifuko hivyo kuna haja ya watumishi
kutoka taasisi zote zinazo jihusisha na masuala ya Mikopo na Programu
kuwatembelea wananchi na kutoa elimu juu ya Mifuko hiyo.
Dismas alisema kuwa elimu sahihi haijatolewa ili kubaini
fursa ili watu waelewe njia ya kupata mikopo kupitia mifuko inayo toa kwa jili
ya kuwawezesha wananchi kiuchumi.
‘Watu bado wanamitazamo tofauti kuhusiana na maonesha wengi
wanadhani ni kwa ajili ya kuja kula nyama au kunywa hivyo kuna kazi kubwa
lakini.. Mifuko inayotoa mikopo haijawajibika ipasavyo na ndiyo maana wananchi
hawaelewi’ alisema Dismas.
Alisema kuwa Mifuko hiyo inawajibu wa kutoka ofisini na
kuwafuata wananchi waliko ili kwenda kutoa mawazo na kuibua fursa za kiuchumi badala
ya kuwasubili kufutwa ofisini.
Aidha katika hatua nyingine Yusuph aliwataka wazalishaji na
wasindikaji wa bidhaa mbalimbali kutumia majina ya bidhaa kwa lugha ya Kiswali,badala
ya Kiingeleza kama ambavyo wengi wao wanatumia kwani kufanya hivyo wanajitenga na
soko.
‘Elimu inahitajika sana mfano watu wanatumia lugha ya Kiingeleza
kuita majina ya bidhaa wanazo zalisha kufanya hivyo ni kujitenga na soko hivyo
niwasii wasindikaji watumie lugha Kiswahili kwenye bidhaa zinazozalisha’
alisema Dismas.
Naye Nkurugenzi wa Taasisi ya (PASS) Nicomed Bohay alisema
alisema suluhisho soko ya mazao ya kilimo lipo mikono mwa wakulima wenyewe kwa
kubuni aina ya aina gani ya bidhaa wanaweza kuzalisha kutoka na mazao wanayo
zalisha.
‘Mwarobaini wa soko la mazao ya wakulima ni wakulima wenyewe kwa kubuni bidhaa watakazo zalisha kutumia mazao wanayo
zalishwa kwa mfano Mahindi unaweza kuzalisha chakula cha mifugo’ alisema
Nicomed




No comments:
Post a Comment