Mshindi wa mbio za Nagai City International Marathon kwa wanawake, Angel John, akishangilia na bendera ya Taifa jana. Mbio hizo zilifanyika jijini Nagai Japan. (Na Mpiga Picha Maalum).
NA SALUM MKANDEMBA
WANARIADHA
wa Tanzania wameng’ara vilivyo katika Mbio za Kimataifa za Jiji la Nagai nchini
Japan (Nagai City International Marathon 2018), baada ya kushika nafasi zote za
juu katika Kilomita 42 na 21 (Wanawake na Wanaume).
Tanzania
imewakilishwa na wanariadha nane katika Mbio za Nagai City International
Marathon, zilizofanyika leo jijini Nagai, Japan, ambako Marco Joseph wa Talent
Athletics Club ya Arusha, aliibuka mshindi kwa upande wa wanaume kilomita 42
akitumia saa 2:21:13.
Katika
mbio hizo, Marco amefuatiwa na Wilbardo Peter wa
klabu ya Polisi, aliyekimbia kwa saa 2:32:12, ambako ukiondoa zawadi, Marco
alitwaa Medali ya Fedha, huku Wilbardo akitwaa Medali ya Fedha ya mbio hizo.
Kwa
upande wa mbio za kilomita 42 Wanaume, Tanzania pia imeng'ara, baada ya
Angelina John Yumba wa Talent Athletics Club kushinda akitumia saa 2:43:21,
muda ambao umemuwezesha kufuzu kushiriki Mashindano ya Dunia yatakayofanyika
Doha, Qatar mwakani.
Kasi
ya Watanzania haikuishia hapo tu, kwani moto wao uliendelea kuunguza wapinzani
hadi kwenye nusu marathon km 21 kwa wanaume, ambako Fabiano Nelson Sulle wa
klabu ya Polisi, ameshinda akikimbia kwa saa 1:02:53.
Kwa
upande wa wanawake km 21, Tanzania iliendelea kutikisa, baada ya nafasi zote
nne za juu kubebwa na Watanzania, ambako Amina Mohamed Mgoo ameshinda kwa kutumia
saa 1:16:08, akifuatiwa na Rozalia Fabian Duye 1:18:57 (wote wakitokea klabu ya
JKT).
Naye
Sylivia Masatu wa Maranatha Athletics Club ya Arusha, ameshika nafasi ya tatu akikimbia
kwa muda wa saa 1:32:52, huku Neema Paulo wa Talent Athletics Club, akishika
nafasi ya nne kwa muda wa saa 1:41:36.
Msafara
huo uliokuwa chini ya Katibu Mkuu wa zamani wa Baraza la Michezo la Taifa
(BMT), Mohamed Kiganja, unatarajiwa kurejea nchini Jumatano Oktoba 24.





No comments:
Post a Comment