HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

February 05, 2019

WAKENYA WAFURAHIA JINSI DAWASA ILIVYOJIPANGA KUWAPA HUDUMA KWA WANANCHI

Mkurugenzi wa uzalishaji na usambazaji maji wa DAWASA, Mhandisi Aron Joseph akifunga warsha kwa ajili ya kujifunza masuala mbali mbali yanayohusu Miradi ya MajiTaka kwa wageni waliofika katika warsha ya siku moja ya kujengeana uwezo baina ya TANZANIA NA KENYA juu ya mafanikio na changamoto zinazowakabili. Wageni hao ni maofisa wa Serikali ya Kenya kutoka Kampuni ya Majisafi na Majitaka Nairobi (NCWSC) na Huduma za jamii, Mashirika binafsi na viongozi wa vikundi vya jamii ambao walikuja nchini Tanzania kwa siku 5 wakitembelea Dar es Salaam na Mwanza. Picha zote na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG.
Mkurugenzi wa Shirika lisilo la Kiserikali linalojishughulisha na masuala ya Kijamii nchini (CCI) Tim Ndezi akiwatambulisha wageni kutoka nchini Kenya waliofika Tanzania kwa ajili ya kujifunza masuala mbali mbali yanayohusu Miradi ya MajiTaka kupitia Shirika la CCI na Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka (DAWASA) katika warsha ya siku moja ya kujengeana uwezo baina ya TANZANIA NA KENYA juu ya mafanikio na changamoto zinazowakabili.
Wageni na wenyeji wakifuatilia mkutano huo.
Mhandisi wa Maji na Usafi wa Mazingira wa Shirika lisilo la Kiserikali linalojishughulisha na masuala ya Kijamii nchini (CCI), Festo Dominick Makoba ambaye ndiye msimamizi wa eneo la Vingunguti jijini Dar es Salaam katika mradi wa vyoo vya kisasa kwa wananchi.
Mmoja ya maofisa wa Serikali ya Kenya waliofika Tanzania Bw. Patrick Njoroge wa Akiba Mashirani Trust akielezea hali halisi ya jimbo jipya la Mukuru, Nairobi- Kenya ambalo mipango mji wake haujapangika.
 Bi. Kellen Muchira kutoka Shirika la Caritas Switzerland akizungumza machache.
Msimamizi wa Miradi ya Majitaka Wa Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka (DAWASA) Mhandisi Charles Makoye akiwaelezea juu ya miradi wa kuchakata MajiTaka inayosimamiwa na kuendeshwa na DAWASA kwa wageni kutoka nchini Kenya waliofika Tanzania kwa ajili ya kujifunza masuala mbali mbali yanayohusu Maji Taka kupitia Shirika la CCI.
Mmoja ya wageni kutoka nchini Kenya Nancy akitia shukrani zake za peke kwa DAWASA na CCI kwa kuweza kuwapokea na kuwatembeza kujionea miradi mbali mbali ya MajiTaka jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa Mji Mpya, Kata ya Vingunguti Rahimu Seif Gassi akitoa shukrani kwa wageni kutoka nchini Kenya waliofika Tanzania kwa ajili ya kujifunza masuala mbali mbali yanayohusu Maji Taka kupitia Shirika la CCI na Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka (DAWASA) mara baada ya kumaliza mkutano.
Picha ya pamoja.

No comments:

Post a Comment

Pages