HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

February 05, 2019

TAHARUKI BUNGENI


Leo tarehe 5 Januari, 2018 wakati wa Kipindi cha Maswali na Majibu Bungeni Mwenyekiti wa Bunge, Mheshimiwa Najma Giga, (Mb) alilazimika kusitisha kwa muda Kikao cha Bunge baada ya King’ora cha tahadhari chenye kuashiria hatari kupiga kelele.

Hata hivyo, Wataalam wetu wamefuatilia na kujiridhisha kuwa hakukuwa na tatizo la moto na hivyo Bunge lilirejea na kuendelea na Kikao chake kama kawaida.

Aidha, hakuna madhara yoyote yaliyotokea kwa Waheshimiwa Wabunge, Wafanyakazi wa Bunge wala Jengo la Ukumbi wa Bunge kufuatia taharuki iliyosababishwa na King’ora hicho.

Imetolewa na:-         Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Kimataifa,
 Ofisi ya  Bunge,

 DODOMA.

 5 Februari, 2019.

No comments:

Post a Comment

Pages