HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 27, 2019

RIADHA DAR KUSAKA TIMU JULAI 30

MASHINDANO ya Riadha ya Uwanjani yajulikanayo kama ‘Mzizima Track and Field Championship’ yanatarajiwa kufanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam Juni 30 mwaka huu.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa Chama cha Riadha Mkoa wa Dar es Salaam (DAAA), Kapteni mstaafu Lucas Nkungu, alisema mashindano hayo yameandaliwa na kufadhiliwa na Nyange Mtoro ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa chama hicho.

Nkungu, alisema mashindano hayo lengo lake ni kuibua vipaji na kuhamasisha mbio za uwanjani, ambako pia Mkoa wa Dar es Salaam utayatumia kuchagua timu yake itakayoshiriki mashindano ya Taifa yatakayofanyika jijini Arusha Julai 5 na 6 mwaka huu.

Alisema mashindano hayo yatashirikisha mbio za uwanjani , Kurusha Tufe, Kutupa Kisahani, Kurusha Mkuki, Miruko Mitatu na Kuruka Chini.

Kapteni mstaafu Nkungu, alisema washindi katika mashindano hayo watazawadiwa zawadi za fedha taslimu, ambako wa kwanza atapata Sh. 50,000 wa pili 30,000 na wa tatu 20,000 na pia baadhi yao wataingia katika timu ya Mkoa tayari kwa mashindano ya Taifa.

Alitoa wito kwa klabu, shule na washiriki binafsi kujitokeza kwa wingi na hakuna ada ya ushiriki.

No comments:

Post a Comment

Pages