HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

July 04, 2019

WAZIRI OLE NASHA ATEMBELEA BANDA LA CHUO KIKUU DAR ES SALAAM

Muonekano wa Banda la Chuo Kikuu Dar es Salaam.(Picha zote na Francis Dande).
 Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia William Ole Nasha, akisaini kitabu cha wageni alipowasili katika banda la UDSM.
Kaimu Mkurugenzi Huduma kwa Umma,  Dk. Arnold Towo, akimkaribisha Naibu Waziri wa Elimu Mhe. William Ole Nasha, kwa kumuonyesha kombe alipofanya ziara katika Banda la Chuo Kikuu Dar es Salaam kujionea tafiti zilizofanywa na wataalamu pamoja na wanafunzi wakati wa maonesho ya 43 ya SabaSaba tarehe 3 Julai, 2019.
Naibu Waziri akipata maelezo.
  Dk. Aviti John Mmochi kutoka Taasisi ya Sayansi ya Bahari akimpa maelezo Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia William Ole Nasha, alipotembelea banda la Chuo Kikuu Dar es Salaam.
 Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknoolojia Mhe. William Ole Nasha, akipata maelezo kutoka kwa Safia Hashimu Makame mjasiriamali aliyenufaika na mojawapo ya tafiti ya Kilimo cha mwani iliyofanywa na Chuo Kikuu Dar es Salaam kutoka katika Taasisi ya Sayansi za Bahari iliyopo Zanzibar katika Maonyesho ya 43 ya Biashara ya Kimataifa (DITF) sabasaba.
 Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknoolojia Mhe. William Ole Nasha, akiwa katika banda la Chuo Kikuu Dar es Salaam akipata maelezo kuhusu tafiti mbalimbali.
 Mmoja wa washiriki wa Maonyesho ya 43 ya Biashara ya Kimataifa (DITF), akitoa maelezo kwa Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia katika banda la Chuo Kikuu Dar es Salaam kuhusu tafiti walizofanya.
 

Na Mwandishi Wetu

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia William Ole Nasha ametembelea banda la Chuo Kikuu Dar es Salaam tarehe 3 Julai, 2019 katika Maonesho ya 43 ya SabaSaba yanayoendelea Jijini Dar es Salaam. 
 
Naibu Waziri alipita na kupata maelezo kutoka kwa watafiti mbalimbali akiwemo Dr. Aviti John Mmochi Kutoka Taasisi ya Sayansi za Bahari ya Chuo Kikuu Dar es Salaam kilichopo Zanzibar ambaye alielezea zao la Mwani ambalo mradi huo ulianzishwa na Prof Keto Mshigeni aliyekuwa Idara ya Mimea ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa kusambaza kilimo cha mwani Zanzibar na Bara, kuendeleza utafiti na kuratibu maendeleo yake. 

Kilimo cha mwani kina wakulima zaidi ya 24000 ambao asilimia 80 mpaka 90 ni wanawake. Kwa kuzingatia kuwa bei ya mwani ya shillingi 500 ni ndogo, taasisi pia imesaidia kuanzishwa taratibu za kuongezea thamani na hivi sasa kuna bidhaa nyingi zikiwemo za chakula na vinywaji, vipodozi n.k. vinavyotenezwa na vikundi vya wanawake.

No comments:

Post a Comment

Pages