HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

September 04, 2019

RAIS DKT. MAGUFULI AFUNGUA MKUTANO WA MASHAURIANO WA MWAKA WA AQRB, ERB, CRB PAMOJA NA WADAU MBALIMBALI WA SEKTA YA UJENZI NCHINI, JIJINI DAR ES SALAAM

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia wadau mbalimbali kutoka Bodi ya Usajili Wabunifu na Wakadiriaji Majenzi (AQRB), Bodi ya Usajili Wakandarasi (CRB) Bodi ya Usajili wa Wahandisi (ERB) pamoja na wadau wa  Sekta ya Ujenzi kabla ya kufungua mkutano huo wa Mwaka wa Mashauriano katika Bodi na Taasisi hiyo.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia wadau mbalimbali kutoka Bodi ya Usajili Wabunifu na Wakadiriaji Majenzi (AQRB), Bodi ya Usajili Wakandarasi (CRB) Bodi ya Usajili wa Wahandisi (ERB) pamoja na wadau wa  Sekta ya Ujenzi kabla ya kufungua mkutano huo wa Mwaka wa Mashauriano katika Bodi na Taasisi hiyo.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia wadau mbalimbali kutoka Bodi ya Usajili Wabunifu na Wakadiriaji Majenzi (AQRB), Bodi ya Usajili Wakandarasi (CRB) Bodi ya Usajili wa Wahandisi (ERB) pamoja na wadau wa  Sekta ya Ujenzi kabla ya kufungua mkutano huo wa Mwaka wa Mashauriano katika Bodi na Taasisi hiyo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akikagua vifaa mbalimbali vya Mabomba ya Maji katika viwanja vya Diamond Jubilee mara baada ya kufungua mkutano wa Mashauriano wa Mwaka wa AQRB,CRB,ERB pamoja na Wadau wa Sekta ya Ujenzi nchini.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akikagua vifaa mbalimbali vya Mabomba ya Maji katika viwanja vya Diamond Jubilee mara baada ya kufungua mkutano wa Mashauriano wa Mwaka wa AQRB,CRB,ERB pamoja na Wadau wa Sekta ya Ujenzi nchini.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akikagua moja wapo ya gari linalotumika katika ujenzi wa Miondombimbu mbalimbali katika viwanja vya Diamond Jubilee mara baada ya kufungua mkutano wa Mashauriano wa Mwaka wa AQRB,CRB,ERB pamoja na Wadau wa Sekta ya Ujenzi nchini.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia vitasa mbalimbali vya Milango wakati alipopita kukagua mabanda katika maonesho ya Wadau wa Sekta ya Ujenzi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mchungaji Daniel Mgogo mara baada ya kufungua mkutano huo wa Mashauriano uliofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Charles Kitwanga Mbunge wa Misungwi mara baada ya kukagua mabanda  katika maonesho ya Wadau wa Sekta ya Ujenzi yaliyopo katika viwanja vya Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU.



Na Mwandishi Wetu


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amefungua mkutano wa mashauriano wa wadau wa sekta ya ujenzi hapa nchini na kuwahakikishia Wakandarasi, Wahandisi, Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi kuwa Serikali itaendelea kuchukua hatua madhubuti za kuwajengea uwezo wa kutekeleza miradi mingi na mikubwa hapa nchini.
Mkutano huo wa siku 2 umefunguliwa leo tarehe 04 Septemba, 2019 katika ukumbi wa Diamond Jubilee Jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na wajumbe 4,390 kutoka Bodi ya Usajili wa Wakandarasi (CRB), Bodi ya Usajili wa Wahandisi (ERB), Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi (AQRB) na Wadau wa huduma za bidhaa za ujenzi chini ya kauli mbiu “Wajibu wa wadau wa sekta ya ujenzi katika kufikia uchumi wa viwanda endelevu kwa ustawi wa jamii”.
Katika hotuba yake, Mhe. Rais Magufuli amesema katika kutekeleza sheria inayotaka miradi yenye thamani ya chini ya shilingi Bilioni 10 kutolewa kwa Wakandarasi wa ndani, katika mwaka uliopita miradi 1,068 yenye thamani ya shilingi Bilioni 267.7 iliyotolewa na Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini (TARURA) ilitekelezwa na Wakandarasi wa ndani na kwamba mwaka huu Serikali imetenga fedha nyingine shilingi Bilioni 278.13 kupitia TARURA ambazo miradi yake itatekelezwa na Wakandarasi wa ndani.
Amesema pamoja na kuwapa Wakandarasi wa ndani miradi mikubwa mfano ujenzi wa barabara ya lami ya Rudewa – Kilosa, Urambo – Kaliua na Kimara – Kibaha, Serikali imelipa madeni ya wakandarasi ambapo katika mwaka 2016/17 zimelipwa shilingi Bilioni 557 na mwaka 2017/18 zimelipwa shilingi Bilioni 833.65.
Ameongeza kuwa kampuni za Wakandarasi wa ndani zimeendelea kupata kipaumbele katika utekelezaji wa miradi ya maji ambapo katika mwaka uliopita zimepata miradi yenye thamani ya shilingi Bilioni 386.34 na kwa upande wa miradi ya nishati ya umeme zimepata miradi yenye thamani ya shilingi Bilioni 996.
“Tunafanya hivyo ili kuimarisha uwezo wa wataalamu wetu na kampuni za hapa nchini, na pia kwa lengo la kuhakikisha fedha zetu zinabaki nchini ili zisaidie kuimarisha uchumi wetu” amesema Mhe. Rais Magufuli.
Hata hivyo, Mhe. Rais Magufuli amewakosoa Wakandarasi na Wahandisi hao kwa vitendo vyao vya kutoshirikiana katika utekelezaji wa majukumu na miradi, na ametoa wito kwao kujitafakari na kuchukua hatua zitakazosaidia kuondoa dosari hizo.
Aidha, Mhe. Rais Magufuli amezitaka kampuni za ukandarasi kufanya kazi zao kwa kuzingatia sheria, taratibu na uadilifu wa taaluma yao ikiwemo kujiepusha na vitendo vya rushwa na upangaji wa gharama kubwa za miradi huku akitolea mfano wa uamuzi wa Serikali kujenga majengo yake bila kutumia wakandarasi ili kuokoa fedha nyingi.
“Serikali imejenga vituo vya afya 352 kwa shilingi Bilioni 184, endapo ujenzi huo ungefanywa na Wakandarasi tungetumia shilingi Trilioni 1, ujenzi wa darasa 1 umetumia shilingi Milioni 20 lakini tungetumia Wakandarasi tungejenga kwa shilingi Milioni 50 hadi 60, halikadhalika ujenzi wa bweni bila Wakandarasi umegharimu shilingi Milioni 75 tena likiwa na fenicha lakini tungetumia Wakandarasi tungetumia shilingi Milioni 170, sasa kwa gharama kubwa kama hizi ni lazima mjitathmini na mjirekebishe” amesisitiza Mhe. Rais Magufuli.
Mhe. Rais Magufuli amewataka Wakandarasi hao kuacha kulalamika na badala yake kutumia fursa ya uwepo wa miradi mbalimbali inayotekelezwa hapa nchi kuomba kazi na kuzifanya vizuri na amewahakikishia kuwa changamoto mbalimbali ambazo wameomba zitatuliwe, Serikali itazifanyia kazi.
Ametoa wito kwa taasisi za elimu kuongeza fursa za mafunzo kwa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi ambao amesema idadi yao ni ndogo (chini ya 2,000) ikilinganishwa na idadi ya Watanzania zaidi ya Milioni 50 huku akiwataka Watanzania kuwatumia wataalamu hao katika ujenzi badala ya kujenga holela.
Wenyeviti wa Bodi za CRB, ERB, AQRB pamoja na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu wamempongeza Mhe. Rais Magufuli kwa namna anavyotilia mkazo ujenzi wa miundombinu mikubwa ambayo ni nguzo muhimu ya uchumi hasa tunapoelekea katika uchumi wa kati unaotegemea viwanda na wameahidi kumuunga mkono katika jitihada hizo.
Baada ya ufunguzi wa mkutano huo Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe ametoa tangazo rasmi la Serikali kuwa Ndege ya Tanzania aina ya Airbus 220-300 iliyokuwa ikishikiliwa nchini Afrika Kusini kwa agizo la Mahakama imeachiwa.

No comments:

Post a Comment

Pages