HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

October 24, 2019

COSTECH, ITM wataka uwekezaji tafiti dawa asili

NA MWANDISHI WETU

WATAFITI kutokaTume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) na Taasisi ya Dawa Asili (ITM) wamesema wakati umefika kwa Serikali kuwekeza katika tafiti za dawa asili ili kuweza kukabiliana na magonjwa mbalimbali.
Watafiti hao wamesema hayo jana jijini Dar es Salaam wakati wakizungumza na waandishi wa habari ambao walitembelea ITM iliyopo Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) ikiwa ni muendelezo wa maandalizi ya Mkutano wa Mabaraza ya Utafiti wa Sayansi, Ubunifu na Teknolojia unaotarajiwa kufanyika Novemba 11 hadi 15 mwaka huu jijini Dar es Salaam..
Akizungumza katika mkutano huo Mtafiti Kiongozi wa COSTECH, Dk, Khadija Malima alisema nchi ya Tanzania imejaliwa rasilimali miti dawa mingi lakini hakuna uwekezaji uliowekezwa kuhusu kufikia hatua ya kutengenezwa dawa na kutumika.
Dk. Malima alisema iwapo nguvu itaelekezwa katika uwekezaji wa utafiti wa afya hasa tafiti ambazo zinasaidia wanadamu ni dhahiri kuwa dhana ya Tanzania ya viwanda itatimia,” alisema.
“Sasa tunataka kujiweka sawa katika tafiti za afya hasa zinazomsaidia mwanadamu, ITM imekuwa mnufaika kwa miradi ya utafiti kutoka COSTECH lakini bado uwekezaji haujafanywa wa kutosha kwani Tanzania ina miti dawa mingi ila hajatafitiwa,” alisema.
Alisema haja ya kuwekeza katika eneo hilo ili kuweza kunufaika na maliasili ambazo Mungu ameipatia Tanzania hata kutengeneza dawa katika hatua fulani ambayo inaweza kutoa matumaini,” alisema.
Dk. Malima alisema tafiti nyingi zilikuwa zimejikita kuleta uelewa hivyo ni vema kubadilika ili kuhakikisha tafiti zinafikia hatua ya dawa ili kuweza kuunganisha watafiti na wazalishaji ayaani viwanda.
Alisema matamanio ya COSTECH ni kuona rasilimali zilizopo kupitia wanasayansi zinabadilisha maisha ya binadamu na kuchochea ukuaji wa uchumi wa nchi.
“COSTECH itahakikisha kuwa inawaunganisha watafiti na wenye viwanda hivyo dawa ambazo zimegundulika zitaweza kutibu binadamu, kuwa za kiwango cha juu au za kutosha soko la nchi za Afrika na Kusini mwa Jangwa la Sahara,” alisema.
Mkurugenzi wa Utafiti (COSTECH), Profesa Mohammed Sheikh, alisema majukumu makubwa ya taasisi yao ni kuratibu na kuendeleza utatifi na ubunifu nchini hivyo mkutano huo Mabaraza ya Utafiti ni muhimu kwao kwa kuwahamisisha kufanya tafiti zaidi ili kuweza kunusu wananchi.
Alisema ITM ni taasisi ambayo wamefanikiwa kuiwezesha katika vipindi tofauti kufanya tafiti za dawa mbalimbali ambapo kwa asilimia kubwa matokeo yameanza kuonekana na kwamba mkutano huo utawafungua zaidi.
“Sisi COSTECH majukumu yetu makubwa ni kutafiti na kuendeleza ubunifu nchini hivyo ITM ni kipimo sahihi. Lakini katika mkutano huo kutakuwa na mada tatu ambazo ni kufungua sayansi, kufanya tafiti na ubunifu kuanzia ngazi ya chini na kuachana na tabia ya kufanya kazi wakiwa ofisini ili kuweza kupata taarifa sahihi,”alisema.
Mkurugenzi Mkuu wa ITM, Joseph Otieno alisema kwa miaka zaidi ya 40 ya uwepo wa taasisi hiyo wameweza kudundua miti dawa zaidi ya 12,000 ambapo miti dawa 2,000 zimerikodiwa, 15 zimefanyiwa tafiti na miliwili imeweza kuwa bidhaa.
Alisema uwekezaji katika sekta hiyo ni muhimu ili kuweza kuchochea ya maendeleo nchini kwa kuwa miti dawa ni biashara kubwa duniani ambayo inaweza kubadilisha maisha ya wananchi kiuchumi na kiafya.
“Tanzania ina miti mingi nchini na kati ya hiyo asilimia 25 imefanyiwa utafiti kwa ajili ya matumizi ya dawa mbalilimbali na kwamba iwapo wanataka kuunganishwa watakuwa na pakuanzia.
Otieno alisema miti dawa nchi inaweza kutumika kutengeza dawa bora kutokana na miti hiyo bila kuharibu bioniwayi.

No comments:

Post a Comment

Pages