HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

October 08, 2019

JK azindua msafara waendesha baiskeli kwenda Butiama

  Rais mstaafu wa Awamu ya Nne, Dk. Jakaya Kikwete, akiruhusu msafara wa waendesha baiskeli Msata wilayani Bagamoyo mkoani Pwani jana, ambao utapita katika mikoa saba hadi Butiama mkoani Mara wakienzi kwa vitendo juhudi za Baba wa Taifa. (Na Mpiga Picha Wetu).


Na Mwandishi Wetu
 
KUELEKEA kumbukumbu ya miaka 20 ya hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere tangu kifo chake, Rais Mstaafu Dk. Jakaya Kikwete amezindua msafara wa waendesha baiskeli.

Uzinduzi huo ulifanyika Msata wilayani Bagamoyo mkoani Pwani jana, ambapo waendesha baiskeli hao wanaelekea Butiama kupitia mikoa saba kwa muda wa siku nane wakienzi kwa vitendo juhudi za Baba wa Taifa.

Katika uzinduzi huo, Kikwete amewataka viongozi wa waendesha baiskeli nchini kupanga mipango mikakati ambayo itawasaidia kuendeleza na kukuza mchezo huo kimataifa badala ya kutumia muda wa kuongelea changamoto.

Sanjari na hayo, Dk. Jakaya pia alipanda mti mmoja na kumkabidhi kiongozi wa msafara Gabriel Mlanda mti mmoja ambao utapandwa nyumbani kwa baba wa Taifa, Butiama mkoani Mara.

No comments:

Post a Comment

Pages