HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

October 08, 2019

MAGARI YALIYOTUMIKA CHANZO CHA HEWA UKAA-SIMBACHAWENE

Na Tatu Mohamed

SERIKALI imesema kuna haja ya kupunguza uingizwaji wa magari nchini yaliyotumika ili kupunguza hewa ya ukaa inayochangia ongezeko la joto duniani.

Aidha serikali imesema pia kuna haja ya watu kutumia usafiri wa umma na kuacha matumizi ya magari binafsi kwani na jambo hilo linachangia pia ongezeko la joto na maradhi mengine. 

Hayo yameelezwa leo Oktoba 8, 2019 na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, George Simbachawene katika mkutano wa watafiti na wanasayansi kutoka barani Afrika na nje waliokutana kwa lengo la kujadili changamoto za mabadiliko ya tabianchi na athari zake zilizoanza kujitokeza duniani hasa barani Afrika pamoja na uzinduzi wa kitabu. 

Amesema masuala ya mabadiliko ya tabianchi kwa sasa ni suala la dunia kwani shughuli mbalimbali za kiduniani ikiwemo za viwanda kwa ujumla wake zinasababisha ongezeko la hewa ukaa. 

Ameongeza kuwa, hewa hiyo imepelekea joto kuongezeka duniani hivyo kusababisha misimu kubadilika ambapo madhara yake kutokea mvua kupita kiasi pamoja na ukame.

"Kwasasa tunajaribu kwenda na mabadiliko ni vyema wadau wakashirikiana, na iko haja hata kufundisha mashuleni juu ya mazingira ya mabadiliko ya tabianchi. Magari yanazalisha kaboni monoksaidi, ambayo kwa kiasi kikubwa inaenda kuharibu hozon layer. 

"Hivyo dunia inafikiri katika kuacha kutumia magari yanayochoma Diesel na kuanza yanayotumia umeme, lakini sisi hapa ndo tunaongoza kwa kuingiza magari used, kila mtu anatumia gari lake badala ya kutumia usafiri wa umma kwahiyo iko haja ya kuona kwa mfano kama hapa Dar es Salaam ambapo kuna wingi wa watu,  basi usafiri wa umma ukaboreshwa watu wakatumia huo," amesema Simbachawene. 

Aidha are sema kama tutakubali ongezeko la nyuzi joto kufikia zaidi ya 2 duniani, kwa Africa itabidi kuongeza gharama kwani dola milioni 530 zitahitajika ili kukadiliana na mabadiliko hayo.

"Na kwa hali ya uchumi kwa nchi zinazoendelea tunaweza tukashindwa kuwa na uwezo wa kukabiliana hivyo kusababisha mafaa, na inakadiriwa tukiendelea na hali ilivyo tukaendelea kuharibu mazingira halisi tuliyoachiwa basi tutakuwa na mazingira magumu ya upatikanaji wa huduma mbalimbali za kijamii kutakuwa yaani kutakuwa na uhaba wa kila kitu katika dunia. 

"Kwahiyo nitoe wito watanzania watunze mazingira, vyanzo vya maji, kuacha kukata miti ovyo na kutumia nishati mbadala. Kwa hali ilivyo inatakiwa kuwekeza katika kutunza mazingira ili kupunguza gharama katika kukabiliana na mabadiliko hayo," amesema Simbachawene. 

Naye, Mwenyekiti wa Kigoda cha Mwalimu Nyerere cha Mabadiliko ya tabianchi na mazingira kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Pius Yanda alisema alisema utaweza kibaini maeneo mengine barani Afrika ambayo yatahitaji kufanyiwa utafiti wa mabadiliko ya tabianchi. 

Kuhusu kitabu walichokizindua, alisema  kimeandikwa na wanasayansi watanzania na wa nchi zingine ambacho kimeelezea mabadiliko ya tabianchi hasa katika ukanda wa bahari na kuangalia athari zake na kuonesha jinsi gani utawala bora unaweza ikawa mbinu za kupunguza athari za mabadiliko hayo. 

"Ni kitabu ambacho kinaweza kutumiwa na wapanga sera, wapanga mipango hasa kuhusu uhifadhi wa mazingira, ni kitabu ambacho tunaweza kujivunia," alisema Profesa Yanda.

No comments:

Post a Comment

Pages