Wafanyakazi
wa Benki ya NMB Kanda ya Kati wakiangalia mashuka na wafanyakazi wa
Hospitali ya Wilaya ya Kiteto Mkoani Manyara muda mfupi baada ya benki
hiyo kukabidhi msaada wa vifaa
tiba wenye thamani ya zaidi ya milioni tano hospitalini hapo.
Baadhi ya Wananfunzi wa Shule ya Sekondari ya Chief Sarwat ya Wilaya ya Mbulu Mkoani Manyara wakibeba viti na meza muda mfupi
mara baada ya kukabidhiwa msaada huo na Benki ya NMB wenye thamani ya shilingi milioni tano shuleni hapo.
Na Mwandishi Wetu
Benki ya NMB imetoa msaada wa madawati 215 katika shule za sekondari Mahenge, Vigoi na Isongo zilizoko Wilayani Ulanga mkoa wa Morogoro na Ng’hoboko iliyoko Wilayani Meatu Mkoani Simiyu.
Mbali
na hilo benki hiyo pia imetoa msaada wa vifaa tiba katika hospitali ya
Wilaya ya Kiteto vyenya thamani ya shilingi milioni tano ambapo vifaa
hivyo vilivyotolewa ni pamoja na vitanda
na mashuka na magodoro.
Msaada
huo wa madawati umegharimu kiasi cha sh. Milioni 20, ambapo katika
shule za Wlaya ya ulanga benki hiyo imetoa madawati 165 yaliyogharimu
Milioni 15 huku katika shule ya Ng’hoboko imetoa
madawati 50 ambayo yamegharimu Milioni 5.
Vifaa
hivyo pamoja na madawati vimetolewa kwa nyakati tofauti ndani ya wiki
hii, ambapo vinaifanya benki hiyo kuchangia katika shughuli za maendeleo
jumla ya shilingi Milioni 675 hadi sasa
kwa mwaka huu tu.
Meneja
wa benki hiyo kanda ya Magharibi Sospeter Magesse akiongea katika hafla
ya kukabidhi madawati shule ya Ng’hoboko alisema kuwa msaada huo
umetolewa ili kuwawezesha wanafunzi wasome vizuri.
Alisemakuwa
benki hiyo imekuwa ikitenga kiasi cha sh. Bilioni moja kila mwaka kwa
ajili ya kurejesha kwa wananchi, pesa ambayo imekuwa ikitumika kuboresha
huduma za elimu, na afya.
“
NMB kama benki ya watanzania itaendelea kusaidiana na serikali pamoja
na watanzania katika kuboresha huduma za afya na elimu, tuna imani kwa
msaada huu wanafunzi watajisomea vizuri,”
alisema Magesse.
Naye
Nsolo Mlozi Meneja wa benki hiyo kanda ya kati akikabidhi vifaa tiba
katika hospiali hiyo alisema kuwa NMB inatoa msaada huo kama njia ya
kurudisha faida kwa wananchi ambao ndiyo wateja
wao wakubwa.
“
Ingawa Serikali inafanya makubwa, Benki hiyo inao wajibu wa kuunga
mkono juhudi hizo za maendeleo kwa kusaidia jamii kwani kupitia jamii
hii hii, ndio imeifanya benki NMB kuwa hapa
ilipo na kubwa kuliko benki yoyote hapa nchini,” Alisema Mlozi.
“
Vifaa hivi vya tiba na afya tunavyokabidhi leo ni moja ya ushiriki wetu
katika maendeleo ya jamii na sisi kama benki inayoongoza Tanzania
tunahakikisha jamii inayotuzunguka inafaidika
kutokana na faida tunayoipata,” aliongeza Mlozi.
Mkuu
wa Wilaya ya Ulanga Mkoani Morogoro Ngolo Malenya akipokea madawati
ameishukuru benki ya NMB kwa kutoa madawati 165 kwa ajili ya wanafunzi
wa shule za sekondari za mahenge ,vigoi
na isongo
Ametoa
wito kwa wanafunzi hao kuwa mabalozi kwa wazazi wao kwa kuwaeleza
mambo mazuri yanayofanywa na benki hiyo ili pia wazazi hao waiunge
mkono benki hiyo kwa kufungua account mbalimbali
ili NMB izidi kurudisha faida wanazopata kwa jamii kwa kuleta
maendeleo.
Naye
Mkuu wa Wilaya ya Meatu Dk. Joseph Chilongani, aliishukuru benki ya NMB
huku akitaka wanafunzi wa shule hiyo na walimu kuhakikisha madawati hayo
yanatunzwa ili kudumu kwa muda mrefu.
“
Kuna haja ya kuweka adhabu kidogo kwa wale ambao watahusika kuaribu
haya madawati, akiaribu mwanafunzi yeye au mzazi wake wahusike katika
kutengeneza, tunataka haya madawati yatumiwe
na wadogo zetu ili waone umuhimu wa NMB,” alisema Chilongani.
No comments:
Post a Comment