HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

October 01, 2019

RAIS MHE. DKT. JOHN POMBE MAGUFULI AMUAPISHA MKURUGENZI WA TUME YA UCHAGUZI (NEC) PAMOJA NA MKUU WA ITIFAKI (CHIEF OF PROTOCAL) IKULU JIJINI DAR ES SALAAM

Ikulu, Dar es Salaam
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 01 Oktoba, 2019 amemuapisha Dkt. Wilson Mahera Charles kuwa Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na Kanali Wilbert Augustine Ibuge kuwa Balozi.
Hafla ya kuapishwa kwa viongozi hao imefanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na Makamu wa Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji) Mhe. Angellah Kairuki na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Mhe. Jaji Mstaafu Semistocles Kaijage.
Akizungumza baada ya kuwaapisha, Mhe. Rais Magufuli amewatakia heri viongozi walioapishwa na kuwataka wafanye kazi kwa kumtanguliza Mwenyezi Mungu na kwa maslahi ya Taifa.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Dkt. Wilson Mahera Charles kuwa Mkurugenzi wa Tume ya Uchaguzi (NEC), katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam.
Kanali Wilbert Augustine Ibuge akila Kiapo cha  kuwa Balozi Ikulu jijini Dar es Salaam.

 Picha namba 3. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Kanali Wilbert Augustine Ibuge kuwa Balozi ambaye ameteuliwa leo kuwa Mkuu wa Itifaki Chief of Protocol wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha na Makamu wa Rais Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan pamoja na Mkurugenzi wa Tume ya Uchaguzi (NEC) Dkt. Wilson Mahera Charles wa kwanza kushoto na Mkuu wa Itifaki (Chief of Protocol wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Wilbert Augustine Ibuge. Wengine katika picha ni Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe, Katibu Mkuu Ikulu Dkt. Moses Kusiluka, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji) Angellah Kairuki pamoja na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC ) Jaji Mstaafu Semistocles Kaijage. PICHA NA IKULU.

No comments:

Post a Comment

Pages