Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 01
Oktoba, 2019 amemuapisha Dkt. Wilson Mahera Charles kuwa Mkurugenzi wa Tume ya
Taifa ya Uchaguzi (NEC)
na Kanali Wilbert
Augustine Ibuge kuwa Balozi.
Hafla
ya kuapishwa kwa viongozi hao imefanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam na
kuhudhuriwa na Makamu wa Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan, Waziri wa Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe, Waziri wa Nchi, Ofisi
ya Waziri Mkuu (Uwekezaji)
Mhe. Angellah Kairuki na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Mhe. Jaji
Mstaafu Semistocles Kaijage.
Akizungumza baada ya kuwaapisha, Mhe. Rais Magufuli
amewatakia heri viongozi walioapishwa na kuwataka wafanye kazi kwa kumtanguliza
Mwenyezi Mungu na kwa maslahi ya Taifa.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Dkt. Wilson Mahera Charles kuwa Mkurugenzi wa Tume ya Uchaguzi (NEC), katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam.
Picha namba 3. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt.
John Pombe Magufuli akimuapisha Kanali Wilbert Augustine Ibuge kuwa
Balozi ambaye ameteuliwa leo kuwa Mkuu wa Itifaki Chief of Protocol wa
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Ikulu jijini
Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe
Magufuli akiwa katika picha na Makamu wa Rais Mheshimiwa Samia Suluhu
Hassan pamoja na Mkurugenzi wa Tume ya Uchaguzi (NEC) Dkt. Wilson Mahera
Charles wa kwanza kushoto na Mkuu wa Itifaki (Chief of Protocol wa
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Wilbert
Augustine Ibuge. Wengine katika picha ni Waziri wa Habari, Utamaduni na
Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe, Katibu Mkuu Ikulu Dkt. Moses Kusiluka,
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji) Angellah Kairuki pamoja
na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC ) Jaji Mstaafu
Semistocles Kaijage. PICHA NA IKULU.
No comments:
Post a Comment