HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

January 14, 2020

BAO LA MTIBWA LAUWASHA MOTO MSIMBAZI, MO NJIA PANDA

  
Na Mwandishi Wetu

UTAMU wa maneno ni kuweza kuyaishi kwa vitendo, ikiwa kinyume huleta dhahama. Ndivyo imekuwa kwa Simba SC baada ya kupoteza  taji la kwanza msimu huu kwa kukubali kipigo cha bao 1-0 mbele ya Mtibwa Sugar, katika fainali ya Kombe la Mapinduzi.

Mchezo huo ulilindima jana  usiku kwenye Uwanja wa Amaan Visiwani Zanzibar, ambapo Simba ikiwa na mastaa wake tegemeo ilionekana mdebwedo katika kila idara na Mtibwa Sugar, ambao waliingia fainali baada ya kuichapa Yanga kwa mikwaju ya penati huku Simba nayo ikiwaondoa mabingwa watetezi, Azam FC.

Kipigo hicho kimeacha maumivu na mateso kwa mashabiki wa Simba ambayo yameongezewa chachandu ya moto na kuchoma zaidi baada ya Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa klabu hiyo, Mohammed Dewji (Mo) kutangaza kuachia ngazi kutokana na kutoridhishwa na matokeo hayo.

Katika taarifa yake kupitia ukurasa wake wa Twitter muda mfupi baada ya kumalizika kwa mchezo huo, Mo alisema: 
“Baada ya kulipa mishahara inayofikia Sh4 bilioni kwa mwaka, najiuzulu wadhifa wa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi. Nitabaki kuwa mwekezaji na nitazingatia kukuza miundombinu ya soka la vijana.” aliandika Mo.

Mtibwa ambao walionekana kucheza soka safi na kumiliki mchezo huo, ilipata bao lake la ushindi dakika ya 38 kupitia kwa Awadh Salum, ambaye alipenya katikati ya msitu wa walinzi wa Simba.

No comments:

Post a Comment

Pages