HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

January 04, 2020

KAIMU KATIBU MKUU DKT.ALLY POSSI: BAKITA ONGEZENI MATUMIZI YA KISWAHILI KATIKA MTANDAO

 Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni , Sanaa na Michezo Dkt.Ally Possi (kushoto ) akizungumza na wafanyakazi wa Baraza la Kiswahili la Taifa (hawapo pichani) kuhusu kuongeza ubunifu wa miradi ya kusambaza kugha ya Kiswahili katika mifumo ya Tehama  leo jijini Da es Salaam alipotembelea ofisi hiyo,Kulia ni Katibu Mtendaji  BAKITA Dkt.Selemani Sewangi.
 Katibu Mtendaji  Baraza la Kiswahili la Taifa  Dkt.Selemani Sewangi  (kulia) akitoa ombi kwa Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni , Sanaa na Michezo Dkt.Ally Possi (kushoto) la kuomba wizara  kuwasaidia fedha za kununua vifaa vya kufundishia  ukalimani alipomtelea ofisini kwake  na kufanya kikao na wafanyakazi leo jijini Dar es Salaam.
 Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni , Sanaa na Michezo Dkt.Ally Possi (kulia) akipokea zawadi ya Kamusi Kuu ya Kiswahili  iliyoandaliwa na Baraza la Kiswahili la Taifa kutoka kwa Katibu Mtendaji  Baraza la Kiswahili la Taifa  Dkt.Selemani Sewangi leo Jijini Dar es Salaam alipotembela ofisi hiyo kwa lengo la kufuatilia utekelezaji wa majukumu.
 Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni , Sanaa na Michezo Dkt.Ally Possi (kulia) akikagua majengo ya ofisi za Baraza la Kiswahili la Taifa alipotembelea ofisini hapo leo Jijini Dar es Salaam kwa lengo la kufuatilia utekelezaji wa majukumu, kushoto  ni  Katibu Mtendaji  Baraza la Kiswahili la Taifa  Dkt.Selemani Sewangi.

 Mfasiri Mkuu wa Baraza la Kiswahili la Taifa Bibi.Vidah Mutasa akitoa neno la shukrani kwa niaba ya  wafanyakazi  wenzake  kwa  Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni , Sanaa na Michezo Dkt.Ally Possi  mara baada ya kumalizika kwa kikao na kiongozi huyo katika ofisi za baraza leo Jijini  Dar es Salaam.
Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni , Sanaa na Michezo Dkt.Ally Possi (wa tatu kulia) akiwa  katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Baraza la Kiswahili la Taifa  alipotembelea  ofisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam (watatu kushoto) ni Katibu Mtendaji  Baraza la Kiswahili la Taifa  Dkt.Selemani Sewangi. (Picha na Anitha Jonas – WHUSM, Dar es Salaam).

No comments:

Post a Comment

Pages