HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

January 01, 2020

TAMWA WAVISHAURI VYAMA VYA SIASA

Na Mauwa Mohammed, Zanziibar

Mkurugenzi wa chama cha Wandishi wa Habari Wanawake Zanzibar (TAMWA), Dkt. Mzuri Issa, amevitaka vyama vya siasa kuwandaa wanawake ili waweze kugombea nafasi za tofauti za uongozi.

Akizungumza na wadau wa vyama vya siasa wakati wa kuwasilisha ripoti ya utafiti iliyofanywa kwa vyama vya siasa ili kubaini  changamoto zinazowakwaza wanawake  katika kugombea nafasi za uongozi.

Mkurugenzi huyo alisema katika vyama vya siasa kuna mapungufu mengi ambayo yanamkwaza mwanamke na kupelekea kushindwa kugombea nafasi za uongozi.

Akiwasilisha ripoti hiyo Edi Issa kutoka Youyth Foroum alisema wanawake wanakabiliwa na changamoto ya tamaduni, silka ,hali ya uchumi kuwa duni  pamoja na wanawake wenyewe  kutokujitambua na kupelekea  kushindwa kugombea nafasi za uongozi.

Alisema mfumo wa vyama vingi unaonekana ni uadui wakati Tanzania imo  katika mfumo wa vyama vingi na pia wanawake wasomi hawako tayari kuingia kwenye siasa kutokana na kukosa mashirikiano kutoka kwa jamii.

Aidha alisema pia wanawake wanakumbwa na changamoto ya ukosefu wa rasilimali fedha  na woga wa kutolewa kashfa zinazoweza kumvunja moyo wakati anaposimama mbele kwa nia ya kujieleza.


Wakichangia washiriki wa mkutano huo walisema wanawake wanaotaka kugombea nafasi wapewe elimu ili wapate kujielewa na pia wanaume na wao wajengewe uwezo ili na wao waweze kujua umuhimu wa viongozi wanawake.

Akiwasilisha mazimio ya mkutano huo Afisa Sera na utafiti wa TAMWA Haura Shamte amesema Tanzania imeridhia mikataba mingi ya kimataifa  ikiwemo   azimio la SADEC linalosema ifikapoi 2030 tayari kila nchi iwe  imefikia asilimia 50% ya wagombea wanawake katika nafasi za uongozi.

“Kwa kuanzia mwaka 2020 kuwepo mikakati angalau  iwe tayari imeshafikia angalau asilimia 40 iwe wanawake wamegombea    kwenye nafasi za uongozi wa mabunge na wawakishi ili kufikia malengo ya mkataba huo”alisema Bi Haura.

Pia serikali imetakiwa kuweka mazingira rafiki na salama kwa wagombea inapofika wakati wa uchaguzi ili wagombea wanawake waondoshe  hofu na woga katika kugombea nafasi hizo.


“tunaviomba Vyama vitoe vipeperushi ili kumpa kipaumbele mwanamke anapogambea achaguliwe” alisema Haura.

Bi haura akitoa maoni kwa niaba ya Tamwa alishauri  kufanywe mapitio ya Muongozo wa kamati ya madili ili kulinda mwanamke na suala la ukatili na udhalilishaji akiwa mgombea au kampeni meneja na ziwepo kanuni  ili kuona mwanamke analindwa katika siasa na  wakati wa uchaguzi.

“Imeonekana vyama vya siasa havitoi nafasi muafaka kwa watu waliopembezoni wakiwemo wanawake na watu wenye ulemavu  hivyo Vyama vya siasa vijipange vitoe nafasi kwa watu wenye ulemavu wa aina zote” aliendelea Haura.

Tamwa kwa kushirikiana na asasi za kiraiya wameandaa mkakati wa kutafuta changamoto zinowakwaza wanawake ili kuziondoa na badala yake  wapate kugombea  nafasi za uongozi bila woga.

No comments:

Post a Comment

Pages