HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

January 12, 2020

WANANCHI WAMLILIA ALIYEPASUA WAJAWAZITO 1,600 BILA VIFO

Na Mwandishi Wetu, Mlali Dodoma
 
WAKAZI wa Kata ya Mlali waliohojiwa kwa nyakati tofauti wameiomba Serikali Kuu impe haki ya kusikilizwa aliyekuwa Mganga, Henry Gwerino, aliyepasua wajawazito 1,600 bila vifo kufuatia kuondolewa kwenye wa Kituo cha Afya Mlali Utumishi wa Umma kwa madai ya kuwasilisha vyeti vya kughushi!. 
Wengi waliotoa hoja hiyo ni akina mama ambao waliwahi kuwa na matatizo ya akina mama na wengine ujauzito ambao walipasuliwa na kupata mafanikio ya kurejeshewa afya zao, hivyo waliposikia kuondolewa katika utumishi wa umma kwa mganga huyo walitoa neno.
Katika barua yake ya malalamiko ya 05/07/20119 kwa Katibu Mkuu OR kwenye Tume ya Utumishi wa Umma akiomba arejeshwe kazini Gwerino alisema, “Kipindi nipo kazini nimeweza kufanya upasuaji wa dharula kwa akina mama wajawazito zaidi ya 1,600 bila kusababisha kifo chochote”.alisema Gwerino alijenga hoja ili arejeshwe kazini.

Kupitia barua Kumb. Na. HW/KOG/CF.S.20/1VOL.VII/153 YA 11/07/2018 Gwerino alikiri aliandikiwa barua na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa ambayo ilimuondoa kwenye utuminishi wa umma kutokana na kuwakilisha nakala ya cheti cha kughushi cha Kidato cha Nne.
Hata hivyo Wakazi hao walidai, kama zoezi la kuhakiki vyeti liliwahusu wafanyakazi walioajiriwa kuanzia mwaka 2004 kwa mujibu wa Kanuni ya 42 ya Kanuni za Utumishi wa umma za 2003 ikisomwa pamoja na Kanuni D.12 ya Kanuni za kudumu za utumishi wa umma za 2009 katika kuhitimisha Ajira za watumishi, mbona huyu aliajiriwa 1982 na zoezi hilo halimhusu? Waliohoji!.
Pamoja na hoja za wakazi hao, ikumbukwe Gwerino alikiri Katibu Mkuu OR Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala bora katika barua Kumb. Na. CFC.26/205/01/06 ya 13 Aprili 2018 kwa watumishi walioghushi vyeti au kuandika taarifa za uongo katika kumbukumbu zao, aliagiza utaratibu huo ufuatwe katika kusitisha ajira za watumishi.
Aidha Gwerino alidai, mbali ya Tume ya utumishi wa umma kukiri kupokea malalamiko yake kwa barua Kumb.Na CCB.81/125/01/11 ya 05/08/2019 ilimrejeshea Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa suala hili kwa mujibu wa maelekezo rasmi ya serikai yaliyotolewa na Katibu Mkuu, Utumishi kama ilivyorejewa ikimtaka kuwasilisha vielelezo vinavyoonesha namna alivyohitimisha shauri hili, jambo ambalo Gwerino anasema hajapata maelekezo yoyote.
“Tume inasubiri, maelekezo ya ufafanuzi kutoka kwa mwajiri wako. Unatakiwa kusubiri wakati suala linashughulikiwa” alisema hayo ndiyo maagizo aliyopewa lakini alidai hadi leo hajapata maelezo yoyote na wananchi wanasema wanahitaji huduma yake iwasaidie lakini yeye anawataka wawe na Subira.

No comments:

Post a Comment

Pages