Mkuu wa Kitengo cha Kodi Wizara ya Ardhi, Nyumba Maendeleo na Makazi, Denis Masami akizungumza nje ya Kanisa Anglikana Mtakatifu Bernard Buza jijini Dar es Salaam wakati wa ziara ya kuwafuatilia wadaiwa sugu wa kodi ya pango ya ardhi.
Na Asha Mwakyonde
MKUU wa Kitengo cha Kodi Wizara ya Ardhi Nyumba Maendeleo na Makazi Denis Masami amessma kuwa Kanisa Anglikana Mtakatifu Bernard Buza jijini Dar es Salaam linadaiwa kodi ya ya shamba lenye ukubwa wa hekari 410 kiasi cha bil.1.200 tangu mwaka 2005 hadi sasa.
Amesema awali Wizara ya Ardhi Nyumba Maendeleo na Makazi pamoja na Manispaa ya Temeke waliupelekea hati ya madai uongozi wa kanisa hilo
Akizungumza jijini Dar es Salaam Machi 25, mwaka huu katika ziara ya kuwafuatilia wadaiwa sugu wa kodi za pango ya ardhi, Masami amesema kanisa hilo limefunja masharti ya uendelezwaji wa eneo hilo.
Masami amesema kuwa uongozi wa kanisa hilo unafanya biashara kwa kutumia mwavuli wa kanisa na kwamba asilimia 90 wa uendelezwaji wa eneo hilo ni Viwanda.
Amesema taasisi hiyo ya kidini inafanya biashara eneo la kanisa ambapo imepangisha wafanyabiasha wa maduka zaidi ya 200, viwabda, nyumba za kuishi kituo cha mafuta cha Lake Oil Buza huku uongozi huo ukichukua kodi bila kulipa panga la ardhi.
" Tungeweza kuweka kadi hii ya viwanda taasisi ingedaiwa zaidi ya bil.5 hiki kiasi cha bil.1.200 ni kodi ya pango ya ardhi ni kuipotezea serikali mapato," amesema Masami.
Mkuu huyo wa kitengo anaongeza kuwa eneo la kanisa halizidi upana wa mita 50 lakini maaeneo yote ni viwanda na kwamba hakuna sababu ya kanisa hilo kuendelea kulipa kodi ya shamba.
Aidha ametoa rai kwa Ofisa mipango miji ahakikishe wanafanya marekebisho na kuwatoza faini pamoja na kubadilisha matumizi eneo hilo ili walipe kodi stahiki.
Katika hali ya kushangaza uongozi wa kanisa hilo ulikwepa kuongea na mkuu huyo alipotaka kujua ubalishwaji wa matumizi wa eneo husika.
Ametoa wito kwa taasisi zote za Umma na za kidini ambazo zinatumia ardhi kibiashara kulipa kodi ya pango ya ardhi.
Naye Ofisa ardhi Wilaya ya Temeke Erick Asenga amesema kuwa kuanzi Machi 30 mwaka huu wale wote waliokiuka maagizo ya kulipa kodi ya ardhi atawapelekea hati ya madai na kuanza kuwafuatilia.
"Tunawasihi wale wote waliopelekewa hati ya madaj waanze kulipa kwa wakati ili kuepuka mkono wa sheria," amesema Asenga.
Amesema kuwa uongozi wa Kituo mafuta cha Lake Oil Buza wameahidi kupekeka mkataba wao katika Manispaa ya Temeke ili uwezwe kuangalia na kujua aliyewapangisha.
MKUU wa Kitengo cha Kodi Wizara ya Ardhi Nyumba Maendeleo na Makazi Denis Masami amessma kuwa Kanisa Anglikana Mtakatifu Bernard Buza jijini Dar es Salaam linadaiwa kodi ya ya shamba lenye ukubwa wa hekari 410 kiasi cha bil.1.200 tangu mwaka 2005 hadi sasa.
Amesema awali Wizara ya Ardhi Nyumba Maendeleo na Makazi pamoja na Manispaa ya Temeke waliupelekea hati ya madai uongozi wa kanisa hilo
Akizungumza jijini Dar es Salaam Machi 25, mwaka huu katika ziara ya kuwafuatilia wadaiwa sugu wa kodi za pango ya ardhi, Masami amesema kanisa hilo limefunja masharti ya uendelezwaji wa eneo hilo.
Masami amesema kuwa uongozi wa kanisa hilo unafanya biashara kwa kutumia mwavuli wa kanisa na kwamba asilimia 90 wa uendelezwaji wa eneo hilo ni Viwanda.
Amesema taasisi hiyo ya kidini inafanya biashara eneo la kanisa ambapo imepangisha wafanyabiasha wa maduka zaidi ya 200, viwabda, nyumba za kuishi kituo cha mafuta cha Lake Oil Buza huku uongozi huo ukichukua kodi bila kulipa panga la ardhi.
" Tungeweza kuweka kadi hii ya viwanda taasisi ingedaiwa zaidi ya bil.5 hiki kiasi cha bil.1.200 ni kodi ya pango ya ardhi ni kuipotezea serikali mapato," amesema Masami.
Mkuu huyo wa kitengo anaongeza kuwa eneo la kanisa halizidi upana wa mita 50 lakini maaeneo yote ni viwanda na kwamba hakuna sababu ya kanisa hilo kuendelea kulipa kodi ya shamba.
Aidha ametoa rai kwa Ofisa mipango miji ahakikishe wanafanya marekebisho na kuwatoza faini pamoja na kubadilisha matumizi eneo hilo ili walipe kodi stahiki.
Katika hali ya kushangaza uongozi wa kanisa hilo ulikwepa kuongea na mkuu huyo alipotaka kujua ubalishwaji wa matumizi wa eneo husika.
Ametoa wito kwa taasisi zote za Umma na za kidini ambazo zinatumia ardhi kibiashara kulipa kodi ya pango ya ardhi.
Naye Ofisa ardhi Wilaya ya Temeke Erick Asenga amesema kuwa kuanzi Machi 30 mwaka huu wale wote waliokiuka maagizo ya kulipa kodi ya ardhi atawapelekea hati ya madai na kuanza kuwafuatilia.
"Tunawasihi wale wote waliopelekewa hati ya madaj waanze kulipa kwa wakati ili kuepuka mkono wa sheria," amesema Asenga.
Amesema kuwa uongozi wa Kituo mafuta cha Lake Oil Buza wameahidi kupekeka mkataba wao katika Manispaa ya Temeke ili uwezwe kuangalia na kujua aliyewapangisha.
No comments:
Post a Comment