HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

May 07, 2020

WAUZAJI WA NGUO ZA MITUMBA KAGERA WAKIMBIWA NA WATEJA

Baadhi ya wafanyabiashara katika soko la Rwamishenye Manispaa ya Bukoba mkoani Kagera.



Na Lydia Lugakila, Kagera
Wafanyabiashara katika soko la Rwamishenyi mkoani Kagera wametoa kauli hiyo na kueleza kuwa wateja wao wameanza kuikimbia biashara hiyo tangu kulipuka kwa ugonjwa Corona ambapo wateja hao udhani kuwa nguo hizo uenda zinatoka nchi za nje ambazo zimeathirika na mlipuko huo.

Wafanya biashara hao akiwemo Bi Sharifa Abdalla wamesema kuwa hali hiyo ya kukimbiwa na wateja wao imewaathili pakubwa kwani hukumbana na changamoto ya mvua na jua bila kuingiza chochote tofauti na bidhaa hiyo ilivyokuwa ikinunuliwa hapo awali.

Bi sharifa amesema kuwa licha ya changamoto hiyo ya kukimbiwa na wateja kwa kisa ugonjwa was corona bado hawajakata tamaa.

Hata hiyo amewataka wateja hao kutoamini ugonjwa wa Corona katika biashara hiyo kwani bidhaa hiyo imeletwa kabla ya janga hilo.

Hata hivyo ameongeza kuwa wataendelea na biashara hiyo licha ya kuwa ngumu huku wakifuata maelekezo yanayotolewa na wizara ya afya juu ya kujikinga na ugonjwa wa Corona.

No comments:

Post a Comment

Pages