HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 22, 2020

TAMWA ZANZIBAR YAWATAKA WANAWAKE KUCHUKUA FOMU ZA KUGOMBEA

Na Mwandishi Wetu, Zanzibar

Chama cha Waandishi wa Habari Wananawake (TAMWA Zanzibar)  kimewaomba na kuwashauri wanawake wa vyama vyote kuhakikisha wanajitokeza kwa wingi kuchukua fomu za kugombea nafasi hizo.
Ombi hilo limetolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa chama hicho Dt. Mzuri Issa Ali kupitia taarifa yake kwa vyombo vya habari iliyotolewa leo Visiwani Zanzibar.

Alisema kuwa Kwa mujibu wa Sensa ya idadi ya watu na makaazi ya mwaka 2012 Zanzibar ina idadi ya watu wapatao 1,303,569 na kukisiwa kufikia 1,671,598 kwa mwaka 2020 ambapo wanawake ni zaidi ya asilimia 50.
“Hata hivyo uwingi huo wa wetu hauendani na  katika vyombo vya kutunga sheria na kufanya maamuzi na tuliowengi huvunjwa moyo na kupikiwa majungu kwa makusudi wakati wa kugombea nafasi hizo ili hali hiyo isibadilike” alisema Dt. Mzuri.

Alifahamisha kwamba Kutokana na mazingira hayo, ni wastani wa wanawake 200 tu ndio walioteuliwa na vyama vyao kwa Zanzibar kugombea katika maeneo hayo matano ya uchaguzi ya mwaka 2015 ambapo kwa nafasi ya Uraisi iliendelea kutokuwa na mwanamke tokea kurejea kwa vyama vingi.

“ tunawaomba wanawake wajitokeze kwa wingi kutumia haki yao ya kikatiba na pia kuwaongoza wananchi katika nafasi mbali mbali sambamba na wenzao wanaume” alieleza.

Alieleza pia Imekuwa ni kawaida, wanawake kuelekezwa kugombea katika viti maalum tu ambavyo kijinsia huwa havioneshi usawa wa kijinsia na umoja wa wanawake bali huchangia kwa kiasi kikubwa kuleta mgawanyiko wa wanawake.

“Katika uchaguzi uliopita wa mwaka 2015 ni wanawake watatu tu ndio walioweza kuchaguliwa kupitia kwenye majimbo katika nafasi za ubunge sawa na asilimia 6, wawakilishi saba sawa na asilimia 14, madiwani 23 sawa na asilimia 20 na nafasi ya Uraisi ambayo ni moja tu imeendelea kushikiliwa na mwanamme” alieleza Mzuri kupitia taarifa hiyo kwa waandishi wa habari.

Sambamba na hilo TAMWA Zanzibar inaishauri jamii kuwaunga mkono wagombea wanawake ili waweze kuonesha uwezo wao na hivyo kuleta uwiano katika jamii pamoja na maendeleo kwa ujumla.

Wakati huohuo waliiomba  Tume ya Uchaguzi (ZEC) kuweka mfumo maalum wa kupokea maoni kutoka kwa wananchi hasa wanawake wanaokumbwa na udhalilishaji katika kipindi hichi cha heka heka za uchaguzi.

No comments:

Post a Comment

Pages