HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

July 25, 2020

NHC wakabidhi nyumba TFS


Na Mwandishi Wetu

WAKALA wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) wamekabidhiwa nyumba tatu na 
Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) zenye thamani ya shilingi milioni 242.

Akikabidhi  nyumba hizo Mkadiriaji Majenzi wa NHC, Anna Bubelwa alisema nyumba hizo za watumishi wa TFS ni sehemu ya makubaliono ambayo wameingia na wakala huyo kutatua kero ya makazi.

"Mradi huu tunaokabidhi leo sisi kama NHC ni kutokana na mkataba tuliosaini kati yetu na TFS wa kujenga majengo ya watumishi, ofisi za mashamba, ofisi za TFS wilaya na ifisi za Kanda katika kanda sita zilizopo hapa nchini," alisema.

Alisema mradi huu ulianza kutekelezwa  Septemba 2019 na umekamilika kwa asilimia 100 ikiwa ni ujenzi wa nyumba tatu za makazi kwa watumishi ikiwa moja ni ya Meneja wa Shamba la Miti Rubya yenye vyumba vitatu, sebule, choo na jiko na nyumba mbili za watumishi wandamizi..

Mhandisi wa Mradi huo kwa upande wa TFS Kaston Sanga amepongeza serikali kupitia Wakala wa Huduma za Misitu nchini kwa kutenga fedha  kwa ajili ya Kuboresha nyumba za watumishi katika mashamba ya miti nchini.

"Mradi huu wa nyumba za watumishi wa Shamba la Miti Rubya ni kati ya majengo 44 yanayotekelezwa na mkandarasi wa NHC ambapo kwa ujumla wake miradi yote hii imekamilika kwa wasitani wa asilimia 90," alisema  Sanga.

Festo Chaula ni Meneja wa Shamba la Miti Rubya amepongeza juhudi hizi za TFS za kuboresha makazi kwa watumishi wa wakala wa huduma za misitu.

"Binafsi ninashukuru sana kukamilika kwa mradi huu maana tumeteseka sana kwa ukosefu wa  nyumba zenye hadhi kukaa watumishi wa Serikali kwani nyumba tulizokuwa tunaishi hazikuwa na ubora maana zimejegwa mwaka 1982,", alisema Chaula.

Neema Juma ni Mhasibu wa Shamba la Miti Rubya na moja kati ya watumishi  wanaonufaika na mradi huo," alisema.

"Binafsi ninapongeza TFS kutukumbuka na sisi hatimae leo tumekabidhiwa nyumba nzuri zenye hadhi ya kuishi watumishi," alisema  Neema.

Hata hivyo  TFS wanaendelea na mpango wa kuboresha makazi kwa watumishi kwenye mashamba ya miti, Ofisi za Kanda, Ofisi za mashamba na Ofisi za TFS wilaya  kote nchini.


No comments:

Post a Comment

Pages