Chama cha ACT Wazalendo kimepongeza hatua ya utiaji saini Mkataba wa Maelewano baina ya Oman na Serikali ya Umoja wa Kitaifa SUK juu ya ujenzi wa Bandari Jumuishi huko Mangapwani, Kaskazini mwa Zanzibar.
Katibu
 wa Idara ya Habari, Uenezi na Mahusiano Kwa Umma wa Chama Cha ACT 
Wazalendo, Ndugu Salim Bimani amesema."Hii ni hatua kubwa na muhimu kwa 
ajili ya uchumi na  ukuaji  wa Zanzibar inayoongozwa na Rais Dk Hussein 
Mwinyi".
Utiaji saini wa 
makubaliano hayo yaliyofanywa na Katibu Mkuu wa Wizara Ujenzi, 
Mawasiliano na Uchukuzi Bwana, Amour Hamil Bakari na  kwa upande kwa 
upande wa Oman alikuwa ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji cha
 Oman Sheikh Mohammed Al-Tooqi ambaye aliongoza ujumbe kutoka Mamlaka 
hiyo ya Oman. 
Chini ya makubaliano hayo Oman imeweka nia  kujenga 
bandari kadhaa kama vile ya mizigo na makontena, Petroli na gesi, Uvuvi 
na pia kuwepo chelezo kwa ajili ya matengenezo ya meli za ndani na nje 
katika ukanda huu.
Pia 
kuweko eneo la viwanda, eneo la biashara na makaazi ya kisasa, imeelezwa
 na Rais Mwinyi amesema huu ni mwanzo mzuri kwa Zanzibar " Lengo letu ni
 kuleta mabadiliko makubwa kwa maslahi mapana ya nchi yetu na fursa na 
faida kwa watu wote."
Chama
 cha ACT Wazalendo kinawataka wananchi wote wasimame na Serikali ya 
Umoja wa Kitaifa kwa umoja wao iki kuitia hima na shime katika kuijenga 
Zanzibar yetu "Kila tukishikamana ndio tutaipa nguvu Serikali ya Umoja 
wa Kitaifa kufanya kazi na nchi mbali mbali na makampuni mbali. 
Tunaamini mazingira mazuri zaidi yatandikwa kushawishi wawekezaji 
zaidi," alisema Bimani
Pia
 Bimani aliishukuru Serikali na watu wa Oman kudhihirisha uhusiano na 
udugu wa kweli kwa Zanzibar kwa kuweka nia ya mradi huo utakaotoa ajira 
kwa maelfu.
Itakumbukwa Oman imefanya miradi kadhaa
 kikiwemo kilichokuwa Chuo cha Afya cha Mbweni na sasa ni sehemu ya Chuo
 Kikuu cha Zanzibar SUZA na pia Oman inasimamia ujenzi na uhifadhi wa 
Jengo la Beit Al Ajaib ambalo sehemu yake kubwa iliporomoka Disemba 25, 
2020.
 
 
 
 

 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment