HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

July 29, 2021

ZU yawakaribisha wazazi kutembelea Banda la Maonesho ya 16 ya Vyuo Vikuu

 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
Mmoja wa wazazi aliyefika katika banda la Chuo Kikuu cha Zanzibar akipata maelezo na fursa zinazopatikana katika chuo.
 
 
 
Mhadhiri wa Chuo Kikuu Zanzibar Idara ya Biashara- Kitengo cha Uhasibu na Fedha, Dkt. Salama Yusuf.
 
 
 Hussein Ndubikile, Dar es Salaam

Chuo Kikuu cha Zanzibar (ZU) kimewakaribisha na kuwashauri wazazi wenye watoto waliomaliza Kidato cha nne, sita, ngazi za cheti, astashahada na shahada kuhudhuria katika banda lao la Maonesho ya Elimu ya Juu, Sayansi na Teknolojia ili wapatiwe elimu ya  orodha ya kozi zinazofundishwa na walimu na wataalamu wa idara waliobobea.

Hayo yamesemwa na Mhadhiri wa Chuo hicho katika Idara ya Biashara- Kitengo cha Uhasibu na Fedha, Dkt. Salama Yusuf kwenye maonesho hayo yanayoendelea Katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.

Amesema wazazi watakaofika katika banda lao watapata fursa ya kupewa elimu ya kozi zinazowafaa kusoma watoto wao kulingana na ufaulu walionao kutoka kwa walimu na wataalamu wa idara waliopo hapo na kwamba chuo hicho kina mazingira bora ya kujisomea.

" Wazazi wahudhurie hapa bandani watapatiwa  elimu sahihi ya kozi tutoazo zinazowafaa watoto wao tuna walimu na wataalamu waliobobea tuna mazingira bora ya kujisomea watapohitimu watatoka wakiwa mahiri katika taaluma walizosomea," amesema Dkt. Salama.

Amebainsha kuwa katika kuhakikisha wanakabiliana na tatizo la ajira kwa wahitimu chuo hicho kimeanzisha kozi ya ujasiriamali katika ngazi ya  cheti na shahada kuwasaidia wahitimu kujiajiri badala ya kutegemea kuajiriwa.

Amesisitiza kuwa chuo kinazingatia kanuni na miongozo ya wizara ya afya kwani katika maeneo ya chuo hicho kilichopo Tunguu nje ya Mji wa Zanzibar  wanafunzi, walimu na wakuu wa idara wanavaa Barakoa, upakaji vitakasa mikono, ukaaji wa mita moja madarasani pamoja na meneo mengine.

Ameipongeza TCU kwa kuendelea kuandaa maonesho hayo kwani yanatoa fursa adhimu kwa vyuo vikuu na taasisi kujitangaza na utoaji elimu kwa wanafunzi wanaofanya udahili wa masomo wa mwaka 2021/22 huku akiishauri tume hiyo kuboresha mfumo wa mtandao wake ili ufanye kazi kwa haraka.

Dkt. Salama amezitaja kozi mbalimbali zinazofundishwa na chuo hicho katika ngazi mbalimbali ikiwemo Usimamizi wa Biashara, Maendeleo ya Jamii, Sheria, Biashara ya Teknolojia, Ustawi wa Jamii, Uuguzi na Ukunga, Ushauri wa Saikolojia, Masoko, Uhasibu, Sayansi katika Uuguzi,Utawala pamoja na Sanaa katika Uchumi.

No comments:

Post a Comment

Pages