HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

October 21, 2021

MWEGELO ANOGESHA THE GALATICOS DAY


 Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Jokate Mwegelo, akizungumza wakati wa Bonanza la Michezo lililoandaliwa na umoja wa wachezaji wa zamani waliocheza ligi mbalimbali ndani na nje ya nchi. 'The Galaticos'.
Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Jokate Mwegelo, akimkabidhi Kombe nahodha wa timu ya Boko Beach Veterani baada ya kuichapa timu ya Kimomwe katika mchezo wa Fainali ya Bonanza la michezo lilofanyika katika Uwanja wa Gwambina Lounge.    
 

Na Mwandishi Wetu


 Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Jokate Mwegelo amewapongeza Wachezaji wa zamani wa ligi mbalimbali za soka kwa kuandaa Bonaza la mchezo huo lililofanyika Jana jijini Dar es Salaam.

Mwegelo alikuwa Mgeni rasmi wa Bonanza hilo lililofanyika viwanja vya Gwambina Lounge zamani TTC Chang'ombe na kushuhudia mbungu la wakongwe likimwagika vya kutosha.

Alisema michezo ni Afya na ni jambo jema kuona wachezaji wa zamani amabao walisakata kabumbu kwa nyakati zao wanaendelea na michezo jambo ambalo linaendelea kuwafanya wawe na afya njema.

"Kwanza kabisa niwapongeze waandaaji wa Bonanza hilo mmefanya jambo kubwa sana lakuweza kukusanyana na kuweza kukumbushia enzi za ubora wenu naamini hili ni jambo kubwa linalopaswa kuungwa mkono.

Pia alionyeshwa kufueahishwa kuweza kuwashuhudia wakongwe ambao walikuwa na mastaa enzi za uchezaji wao na kuweza kulitumikia taifa kwa uaminifu mkubwa."

Bonanza hilo lilikusanya wachezaji wa zamani hufanyika Kila mwaka mwezi oktoba 14 siku ya kaudhimisha kifo cha Hayati Mwalimu Julius Nyerere.

Wachezaji hao wa zamanj ni muunganika wa wachezaji wa madaraja tofauti ambao wamepata kucheza.

Lengo la kuanzishwa kwao umoja wa wachezaji wa zamani The Galaticos ni kuweza kuwa pamoja katika kusaidiana katika shida na Raha Ili kuenzi undugu na Urafiki pamoja na kuenzi utumishi wao katika Soka.

Vilevile ni kuweza kukutana na kuzungumza Juu ya muelekeo wa Soka la Nchi kwa kutoa ushauri pale unapohitajika.

Nae Mwenyekiti wa wachezaji wa zamani Ally Mayay alisema umoja huo umekuwa nguzo ya kutatua changamoto za wachezaji wa zamani na kuwaweka pamoja .

"Bonanza la wachezaji wa zamani ambalo limetufanya wachezaji wastaafu kucheza soka kwenye madaraja tofauti, siku za mwanzo tulikuwa wachezaji wa ligi Kuu tu lakini baadae tukasema hata wachezaji walio cheza daraja la kwanza hata kama la tatu ilimradi tu ligi iliyokuwa inatambulika" alisema na kuongeza kuwa

"Hili tumelifanya baada ya kuona wachezaji wengi wanaishi kinyonge baada ya kustaafu, kwaiyo tukatengeneza kitu ambacho wenyewe tutakuwa tunajitegemea, na kiukweli toka tumeanzisha umoja huu kuna misiba mingi sana ambayo watu wamesaidiana, kwa mfano mchezaji akifiwa na Baba, Mke sijui Mtoto anapewa Milioni moja, lakini anapswa kuwa mwanachama hai ambaye analipa Ada, analipa michango ya misiba lakini pia wanasaidia Ada za wachezaji ambao wanataka kusomea ukocha, mechi kamishina kwaiyo umoja huu unasaidia sana"

"Umoja huu umewafanya wachezaji kuwa pamoja walikuwa wanaalikwa tu kwenye mabonanza, likubwa ukaribu na kuanzia mwenyekiti mpaka mjumbe Wote ni Wachezaji wa zamani, kwaiyo haujachukua mtu ambaye ni nje ya wao wenyewe. Kama watakosea kujiongoza ni wao wenyewe. Alisema Ally Mayay Mwenyekiti wa Wachezaji wa zamani The Galaticos.

No comments:

Post a Comment

Pages