HABARI MSETO (HEADER)


January 29, 2022

Dk.Gwajima ashiriki mazishi ya mtoto alichomwa kisu



 Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia wanawake na Makundi Maalum Dk. Gwajima akiweka shada wakati wa msiba wa kijana Egidi Gangata, aliyefariki dunia kwa kuchomwa na kisu jijini Dodoma.



Na Asha Mwakyonde, Dodoma


VIONGOZI ngazi ya mkoa na halmashauri, kata, mitaa, kijiji na vitongoji  wametakiwa kujipanga upya kutekeleza mwongozo ambao ulizinduliwa wa Mpango Kazi wa Kupambana na Ukatili wa Wanawake na Watoto (MTAKUWWA).

Mwongozo huo ulizinduliwa mwaka  2017/2018 ambao umeelekeza kuundwa kwa Kamati za Mapambano kuanzia Kitongoji, Mtaa, Kijiji, Halmashauri, Mkoa na Taifa.
Pia  serikali itachukua hatua zote dhidi ya waliohusika na kusababisha kifo cha myoto huyo.

Hayo yalisemwa jijini Dodoma leo na Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wanawake na Makundi Maalumu Dk. Dorothy Gwajima kwenye msiba na mazishi ya Marehemu Egidi Gangata aliyekuwa akishi mitaani  aliyefariki kwa kuchomwa kisu maeneo ya Nyerere Square jijini hapa Dk. Gwajima amesema  wadau wote waliopo ngazi husika wakijielekeza kupambana na mifumo inayosababisha kujitokeza kwa ukatili ikiwemo inayopelekea watoto kuishi mitaani.

Dk. Gwajima ameeleza kuwa
 serikali itachukua hatua zote dhidi ya waliohusika na kusababisha kifo cha myoto huyo.
Mwanga wa Milele Umwangazie Eee Mungu, apumzike kwa Amani Milele, Amina.

Amesema tukio hilo na mengine ya aina hiyo yanadhihirisha haja ya Kamati hizi kuongeza kasi ya kufanya kazi.

 "Natoa wito kwa wadau wote wa maendeleo ikiwemo asasi za kiraia, kidini, sekta binafsi, watafiti, wadau wa maendeleo na jamii  kuungana na serikali kutafuta suluhu ya kudumu inayoendana na mazingira yetu na rasilimali zetu na ubunifu wetu," amesema.

Amesema Wizara itaratibu mkutano wa kitaifa wa wadau kwa lengo la  kupata maoni yao juu ya ufumbuzi wa suala hilo hatimaye wasiwe na watoto wa mitaani badala yake waimarishe mifumo ya makuzi na malezi bora.

Dk. Gwajima amesema wakikubali kuendelea na maisha ya  kuwaona watoto wa mitaani ni kujiandalia hatari mbele kama taifa hivyo lazima wapate ufumbuzi wa kudumu.

"Kifo cha marehemu  Gangata kitupe mtihani tukatafute majibu mapya na mbinu mpya shirikishi. Baada ya salaam hizi, naomba tumwombe Mungu aipumzishe roho ya Marehemu kwa Amani," ameongeza Dk.Gwajima.

Aidha Waziri huyo ametoa wito kwa jamii nzima ya Tanzania, kifo hivho kiwe funzo na wito wa kutuhamasisha kama jamii kuungana ili kuwafikia wengine ambao wanatamani kuishi maisha mapya lakini  wamekosa fursa ambazo zipo ili watimize ndoto zao. 

No comments:

Post a Comment

Pages