HABARI MSETO (HEADER)


January 29, 2022

Maaeneo ya biashara,taasisi,ofisi sasa kuwa na anunani ya makazi

Kaimu  Katibu Mkuu wa  Wizara ya Habari,Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Teddy Njau akizungumza na viongozi wa vitengo wa Shirika la Posta Tanzania wakati  akifingua mafunzo ya kuwajengea  uwezo wa mfumo wa anauani ya makazi.

 

Na Asha Mwakyonde, Dodoma

KAIMU Katibu Mkuu wa  Wizara ya Habari,Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Teddy Njau amewataka
 wananchi,Ofisi pamoja na maeneo yote ya biashara yawe na anuani ya makazi ili kurahisisha zoezi la Sensa ya Watu na Makazi ifikapo mwezi Augosti mwaka huu .

Hayo ameyasema leo jijini Dodoma wakati akifungua mafunzo  ya kujengea uelewa viongozi na Watendaji wa Baraza kuu la Shirika la Posta Tanzania amesema utekelezaji wa zoezi anuani ya makazi ni suala la mtambuka.

Amesema utekelezaji wa anauani za unahusisha wadau mbalimbali ikiwemo wizara,Makampuni mashirika Taasisi serikali na zisizo za serikali na wananchi kwa ujumla.

Ameongeza kuwa umeandaliwa mkakati wa utekelezaji unaoainisha majukumu ya kila mdau katika zoezi zima la utekelezaji wa mfumo huo ikiwemo shirika la posta Tanzania.

"Mfumo huo una manufaa mengi na makubwa katika nyakati hizi za ulimwengu wa digitali kurahisisha uapatikanaji,utoaji na ufikishaji wa huduma au bidhaa pale panapo stahiki kuwezesha kufanyika kwa bisahara za kimtandao ikiwa ni pamoja na kuimarisha ulinzi na usalama.

Kaimu huyo  ameeleza kuwa mfumo  huo wa kidigitali utachangia kutoa fursa kwa vijana kujipatia ajira.

Amesema ni jambo jema kuwajengea uwezo wataalamu kwa lengo la kusimamia uteky wa mfumo huo  wa anuani za makazi.

"Tayari wajumbe wa jumuiya za Serikali ya mtaa(ALAT),makatibu Tawala wa mikoa  na wakuu wa mikoa wote Tanzania Bara wameshapatiwa mafunzo kama haya kwa lengo la kusimamia utekelezaji wa mfumo huu wa anauani za makazi kwa ufanisi," ameeleza.

Amefafanua kuwa kwa upande wa wataalamu wameweza kuwapa mafunzo  wataalamu wa tehama na maafisa mipango miji ramani kutoka Halmashauri zote nchini Tanzania Bara na Zanzibar ambapo walianzimia mpango kazi wa utekelezaji wa mfumo huo katika maeneo yao.

Kaimu posta Masta mkuu Macrice Daniel ameeleza kuwa  wameona ni  kuwakutanisha viongozi wakuu waposta katika mafunzo  ya mfumo wa anuani ya makazi kwa kuwa  Ni mustakabali wa taifa.

No comments:

Post a Comment

Pages