HABARI MSETO (HEADER)


 


Breaking

July 29, 2022

CHUO KIKUU MZUMBE CHATOA MAFUNZO KWA SHIVYAWATA

 

 

Kaimu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe Ndaki ya Dar es Salaam, Dk. Coretha Komba, akitoa hotuba yake wakati wa kufungua mafunzo ya Shirikisho la Vyama vya Watu wenye Ulemavu Tanzania (SHIVYAWATA) Wilaya ya Ubungo jijini Dar es Salaam juzi. Kushoto ni Mwenyekiti wa Shivyawata Wilaya ya Ubungo, Mussa Geuza na kulia ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu Mzumbe Ndaki ya Dar es Salaam, Dk. Feisal Hassan. (PICHA NA FRANCIS DANDE).

 



Mratibu wa Mpango mkakati huo ambaye ni Mhadhili wa Chuo Kikuu Mzumbe Ndaki ya Dar es Salaam, Dk. Feisal Hassan, akizungumza wakati wa mafunzo hayo.



Mweka Hazina wa Shirikisho la Vyama vya Watu wenye Ulemavu Wilaya ya Ubungo, Hemedi Ilumba, akitoa neno la shukrani.
Mwenyekiti wa Chama cha Viziwi Wilaya ya Ubungo,  Simeon Mwakatobe, akitoa neno la shukrani kwa niaba ya wenzake.

 

 Na Mwandishi Wetu


CHUO Kikuu Mzumbe Ndaki ya Dar es Salaam wamekabidhi mpango mkakati wa kuendeleza Shirikisho la Vyama vya Watu wenye Ulemavu Tanzania Wilaya ya Ubungo (2022-2027) huku wakitoa mafunzo namna ya kuutekeleza.


Akifungua Mafunzo hayo Kaimu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe Ndaki ya Dar es Salaam, Dk. Coretha Komba amewataka washiriki kuitumia vema fursa hiyo ili mafunzo hayo yaweze kuwafikia wengi na kuwawezesha kupiga hatua katika nyanja mbalimbali za kimaendeleo.
 
"Tumieni fursa hii vema kwani itakuwa na msaada mkubwa wa kuwainua. Pia ongezeni umakini Ili lengo la semina hii liweze kufikiwa kwa maendeleo chanya na niwatakie mafunzo mema.

Hatua hiyo imekuja mara baada ya Shivyawata'Ubungo' kuomba mafunzo ya utunzaji wa mahesabu, kuandika miradi na mafunzo ya uongozi kutoka kwa Chuo Kikuu cha Mzumbe Ndaki ya Dar es Salaam.

Akizungumza juu ya mkakati huo mratibu wa mkakati huo ambaye ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Mzumbe Ndaki ya Dar es Salaam, Dk. Feisal Hassan amesema walianza kutekeleza mkakati huo baada ya kupokea agizo kutoka kwa uongozi wa Chuo.
 
Amebainisha kuwa wanafunzi ambao wanafanya shahada ya pili ya utawala na menegimenti walikabidhiwa jukumu na wakajitolea kufanya kazi ya kuwasaidia Shivyawata'Ubungo kuandaa mpango mkakati na hilo likawa sehemu ya tathimini ya masomo yao kuweza kuwasaidia kama wanafaulu ama wanafeli.

"Bahati nzuri wakaandaa mpango mkakati mzuri kwa ajili ya kuhusisha kuandaa miongozo ya kutumia na maswali elekezi na vile vile kuwatembelea na kuzungumza na wanaoshirikiana na Shivyawata." Amesema na kuongeza kuwa.

"Leo shughuli inayofanyika ni kuwasilisha kwao huo mpango mkakati, na uwasilishaji huo unafanyika na wao wapo wanatoa maoni yao ya mwisho, baada ya hapo wanakabidhiwa mpango mkakati wao.

"Kuwasilisha mpango mkakati huu ni mwendelezo wa kuwajengea uwezo Ili waweze kujitambua na waweze kutambulika, hivyo kutekeleza majukumu yao vizuri zaidi ukiwa ni mkakati wa miaka mitano (2022-2027).

Akizungumza kwa niaba ya wanafunzi walioshiriki kuandaa mpango mkakati huo Jerome Kihaka, amesema matarajio yao ni kwa upande wa Shirikisho la watu wenye ulemavu Shivyawata'Ubungo kutekeleza yaliyomo kwa mantiki ya kimkakati basi wataweza kufikia malengo.

"Matarajio yetu makubwa ni kwa upande wa Shivyawata kama wataweza kufatisha haya maelekezo ambayo mpango mkakati umetoa kwa maana ya mantiki ya mkakati basi kuna uwezekano mkubwa wa kufikia malengo yao.

"Shirikisho lina dhima yake lakini Ili kuweza kuyafikia yale ni lazima kuwepo kwa mpango mkakati sahihi. Tumeshamaliza kuwaandalia ramani ya kule wanakotaka kufika.

Pia ametoa wito kwa mamlaka za kiserikali kama jeshi la Polisi kuwa na sera ya kuwasaidia katika changamoto zao wanazozipitia huko mitaani sambamba na wadau wengine kuwa nao karibu.

 

 

No comments:

Post a Comment

Pages