Na Hussein Ndubikile, Dar es Salaam
Taasisi
ya Kifedha inayojishughulisha na Utoaji wa Mkopo kwa Watumisi wa Umma
ya BayPort Financial Services imeingia Mkataba na Mhamasishaji wa Klabu
ya Yanga Haji Manara wakua Balozi wa taasisi hiyo ambapo katika kipindi
cha mkataba wake atatumia mitandao ya kijamii kuitangaza taasisi hiyo
kwa jamii.
Akizungumza wakati wa hafla ya utiaji saini wa Mkataba huo huo
mbele ya Wanahabari jijini humo amesema kuwa taasisi hiyo kumpa ubalozi
imempa heshima kubwa na kwa klabu yake ya Yanga pamoja na mpira wa
miguu wa Tanzania kwani ilizieleka kwa wasanii ndiyo waliokuwa wakipata
ubalozi kwenye makampuni mbalimbali.
"Masharti
ya Bayport siyo mwiba Kwa watumishi wa Umma ambao wanalipwa na serikali
pamoja na taasisi zake,hivyo nawasihi wachangamkie fursa hii ,kwani
upatikanaji wa mikopo yao ni rahisi sana na inalipwa kupitia simu ya
kiganjani popote ulipo." Amesema Manara.
Amebainisha
kuwa kutokana na kukua kwa soka la Tanzania na kuheshimishwa ndiyo
sababu taasisi ya BayPort Financial Services imempa ubalozi sababu ya
ushawishi wake katika soka la nchi na jinsi anavyotumia mitandao ya
kijamii.
Amesisitiza
kuwa kuwa taasisi hiyo inatoa huduma zake kwa mujibu wa kanuni za Benki
Kuu ya Tanzania (BOT) na kwa kufuata sheria za fedha hivyo amewashauri
watumishi wa umma kuitumia taasisi hiyo kama sehemu yao ya kupata mikopo
ili kupunguza gharama za maisha.
Ameongeza
kuwa atafanya kazi kwa ushirikiano katika chake chote cha mkataba wake
hivyo atahakikisha watanzania hasahasa watumish hao wanatambua fursa za
mikopo inayotolewa na BayPort.
Amefafanua
kuwa kupitia ubalozi aliopewa na taasisi hiyo atafaidika yeye na kwani
itatoa mikopo kwa wataumishi wa umma na Sereikali kupata mapato.
Amewakumbusha
wachezaji wa mpira wa miguu wenye majina makubwa kutumia mitandao ya
Kijamii kwa ajili ya kujitangaza nakupata kipato kitakachowapunguzia
ugumu wa maisha baada ya kustaafu kucheza mpira.
Ameushukuru
uongozi wa klabu na wadhamini wakw wa GSM kwa kumpa fursa za kuingia
mikataba ya ubalozi na kampuni tofauti bila kumbana
Kwa
upande wake, Afisa Uendeshaji Mkuu wa Bayport ,Nderingo Materu amesema
kuwa taasisi hiyo inatoa huduma za mikopo kwa watumishi wa umma
pekee,ambapo mikopo hiyo inatolewa kwa njia ya mtandao.
Materu
amesema kuwa mteja anayetaka mkopo anapaswa kupiga simu au kubonyeza
*150*49# nakufuata maelekezo ya namna ya kukidhi vigezo vya kupata
Mkopo,hivyo amesema kwamba hakuna haja yakusafiri muda mrefu au kuandika
nyaraka za kuomba Mkopo.
"
Bayport imrahisishia mteja kupata Mkopo Kwa njia ya haraka Kwa njia ya
mtandao,leo tuna mtambulisha Khaji Manara kiwa Balozi wetu kwasababu
tafikisha taarifa zetu Kwa wafuasi wengi wanaomfuatilia kwenye mitandao
yake ya Kijamii ikiwemo Instagram , Tweeter, na Facebook, amesema
Materu.
Nae
Mkuu wa Mauzo wa taasisi hiyo, Lugano Kasambala amesema kwa sasa
wanatoa mikopo ya riba nafuu kwa watumishi wa umma na kwamba wanaweza
kufikiria kutoa kwa watumishi wa sekta binafsi.
Mkuu
wa Kituo cha Mawasiliano ( Call Centre), Mercy Mgongolwa awewashauri
watumishi hao kuchangamkia fursa ya mikopo hiyo kwani inatolewa kwa njia
ya mtandao bila usumbufu wowote.
No comments:
Post a Comment