
Na Hussein Ndubikile, Dar es Salaam
Bodi
ya Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC) imetakiwa kutekeleza majukumu yake
kwa kuzingatia sheria, taratibu, weledi na maadili ya utumishi wa umma.
Aidha,
imetakiwa kutoa miongozo ya thamani halisi ya miradi ya maendeleo
ikiwemo miundombinu ya barabara ili kuokoa fedha za Serikali zinazopotea
kutokana na kukosa miongozo sahihi.
Hayo
yamesemwa jijini Dar es Salaam na Naibu Waziri wa Wizara ya Ujenzi na
Uchukuzi- Sekta ya Uchukuzi Atupele Mwakibete wakati akizindua Bodi Mpya
katika Ofisi za Wakala wa Majengo Nchini (TBA) zilizopo jijijni humo.
Amesema
kuwa kutokana na kukosa miongozo sahihi ya gharama halisi ya miradi ya
maendeleo Serikali imekuwa ikipata kilio cha kuingia gharama tofauti na
awali hivyo ameitaka bodi hiyo kuhakikishia inaondoa changamoto hiyo.
"
Bodi ina jukumu la kuhakikisha thamani ya miradi ya maendeleo inabaki
ileile hii itawezekana mkitekeleza majukumu yenu kwa kufuata na kuweka
mwongozo sahihi wa ujenzi," amesema Naibu Waziri Mwakibete.
Naibu
Waziri Mwakibete ameitaka bodi hiyo kutekekeza majukumu yake kikamilifu
ikiwemo kuleta mabadiliko makubwa katika sekta ya hiyo pamoja na
kuyafanyia kazi mabadiliko yote yaliyoanzishwa.
Ameongeza
kuwa ana imani kubwa bodi hiyo itatekeleza majukumu yake kwani wajumbe
wake wameshapatiwa mafunzo ya utekelezaji na kuikumbusha kuepuka vitendo
vya rushwa na udanganyifu.
Amemuagiza Naibu
Katibu Mkuu Ujenzi kuyasimamia, kuyaratibu na kuyafanyia kazi mabadiliko
atakayoletewa kwa haraka iwezekanavyo ili yaweze kuleta tija
iliyokusudiwa.
Kwa upande wake, Afisa Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Baraza hilo, Dkt Matiko Mturi ameyataja majukumu yake kuwa ni pamoja na kuwezesha maendeleo ya kukua kwa sekta ya ujenzi nchini.
Dkt Mturi ameeleza kuwa jukumu lingine ni kufanya utafiti na kuratibu kufanyika kwa utafiti
utakawezesha
maendeleo katika sekta ya ujenzi lakini pia kuwezesha migogoro
inayotokea katika sekta ya ujenzi hasa kwenye miradi ya ujenzi kupata
utatuzi wa haraka na kuleta tija.
‘Pamoja
na kuwa na mafanikio tumekuwa na changamoto chache ikiwemo ya uhaba wa
wataalamu wa kada za uhandisi,za ukadiriaji majenzi na kada za ubunifu
majengo.
Nae,
Mwenyekiti wa Bodi mpya ya Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC) Dkt Fatma
Mohamed amemuahidi Naibu Waziri kuwa watafanya kazi kwa bidii na ueledi
ili kutimiza majukumu yao ipasavyo ili kuleta mabadiliko katika sekta ya
ujenzi nchini.


No comments:
Post a Comment