Na Mwandishi Wetu, Zanzibar
Mgombea wa Urais Zanzibar kwa tiketi ya CCM ambaye pia ni Rais wa Zanzibar na Menyekiti wa baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi amesisitiza suala la amani wakati wa mkutano wa kampeni wa chama hicho kumnadi mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, uliofanyika viwanja vya michezo, Nungwi mkoa wa Unguja, Kaskazini 18 Septemba 2025.
Akizungumza katika mkutano huo, Dkt. Mwinyi alisema wananchi wanapaswa kuendeleza na kudumisha amani kwani ndiyo msingi wa maendeleo ya taifa letu.
Alisema wananchi wana kila sababu ya kuendelea kuiamini CCM, kutokana na utekelezaji wa kina wa Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2020–2025, ambayo imeleta mageuzi makubwa katika sekta mbalimbali za kijamii na kiuchumi.
"Ninawahimiza wana-CCM na wananchi wote kwa ujumla kujitokeza kwa wingi ifikapo tarehe 29 Oktoba 2025, kushiriki uchaguzi na kuipigia kura CCM ili tuendelee kuimarisha amani, mshikamano na maendeleo ya Zanzibar na Tanzania kwa ujumla" alisema.
Mwenyekiti wa CCM Taifa na Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, alisema kuwa Dkt. Mwinyi ni kiongozi sahihi, mchapakazi, msikivu na hodari, aliye tayari kupewa kipindi cha pili cha kuiongoza Zanzibar kwa kasi zaidi ya maendeleo.
September 19, 2025
Share This
About HABARI MSETO
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Author Details
Ut wisi enim ad minim veniam, quis nostrud exerci tation ullamcorper suscipit lobortis nisl ut aliquip ex ea commodo consequat. Duis autem vel eum iriure dolor in hendrerit in vulputate velit esse molestie consequat.



No comments:
Post a Comment