Na Mwandishi Wetu, Zanzibar
Jumla ya Tsh.Bilioni 61 zimetengwa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) kwa ajili ya fidia kwa watakaopisha ujenzi wa bandari jumuishi ya Mangapwani, mkoa wa Kaskazini, Unguja.
"Fidia hiyo ni kwa wale ambao watataka kulipwa pesa lakini pia ujenzi wa nyumba 54 za kisasa zimekamilika kwa watakaotaka nyumba badala ya pesa" alisema.
Alisema nyumba zilizojengwa serikali imejitahidi ziwe na hadhi kuliko walizotoka.
Mgombea huyo kwa tiketi ya CCM alisema Mangapwani ni kijiji cha bandari kwani kunajengwa sehemu ya meli kushushia mafuta, nafaka na chelezo cha kutengenezea meli.
Miundombinu ya barabara imekamiliki baadhi ya maeneo sanjari na madaraja.
Aliwataka wananchi wa Bumbwini kuilinda amani ili maendeleo zaidi yaweze kupatikana.
Upande mwingine mgombea huyo alisema maboresho yaliyofanywa kwenye sekta ya elimu ufaulu umepanda na akipewa ridhaa anataka ufaulu uwe kwenye daraja la kwanza na la pili na wote wenye sifa wataenda vyuo vya elimu ya juu.
Mkoa wa Kaskazini una shule sita za ghorofa zenye maabara za kisasa, maktaba na madarasa ya kompyuta.
October 03, 2025
Home
Unlabelled
Dkt. Mwinyi: Bilioni. 61 zimetengwa fidia Mangapwani
Dkt. Mwinyi: Bilioni. 61 zimetengwa fidia Mangapwani
Share This
About HABARI MSETO
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Author Details
Ut wisi enim ad minim veniam, quis nostrud exerci tation ullamcorper suscipit lobortis nisl ut aliquip ex ea commodo consequat. Duis autem vel eum iriure dolor in hendrerit in vulputate velit esse molestie consequat.



No comments:
Post a Comment