HABARI MSETO (HEADER)


 


Breaking

April 09, 2026

ABDILATIF ABDALLAH KUIPAMBA TUZO YA TAIFA YA MWALIMU NYERERE YA UANDISHI BUNIFU

WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Adolf Mkenda amesema hafla ya nne ya Tuzo ya Taifa ya Mwalimu Nyerere ya Uandishi Bunifu itafanyika Aprili 13, 2026 kwenye ukumbi wa Super Dome, Masaki  jijini Dar es Salaam. 


Waziri Mkenda ameyasema hayo leo April 9, 2026 jijini Dodoma alipozungumza na Waandishi wa Habari kuhusu tuzo hizo zinazofanyika kila mwaka  amesema, siku ya kumbukumbu ya kuzaliwa Baba wa Taifa, hayati Julius Kambarage Nyerere, 
hafla hii hufanyika kila mwaka kuadhimisha siku ya kuzaliwa kwa Baba wa Taifa la Tanzania, Julius Nyerere na kutambua mchango wake katika kukuza lugha ya Kiswahili na utamaduni wa taifa letu.



Kwa mujibu wa Waziri Mkenda, tuzo za mwaka huu zimehusisha nyanja nne za fasihi ambazo ni riwaya, hadithi za watoto, tamthiliya na ushairi.



"Tunaendelea kukuza Kiswahili, kuendeleza vipaji vya uandishi bunifu, kulinda historia na utamaduni wa taifa na kuongeza hifadhi ya vitabu katika maktaba ndio malengo hasa ya tuzo hii," amesema Waziri Mkenda.


Sambamba na hayo Waziri Mkenda amebainisha kwamba mgeni rasmi katika hafla hiyo ni Mshairi maarufu duniani Abdilatif Abdallah, mwenye asili ya Afrika Mashariki, ambaye aliwahi kufundisha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa zaidi ya miaka 15. 



Hafla hiyo itatanguliwa na mjadala wa kitaaluma utakaoshirikisha waandishi bunifu wa Tanzania na wageni mashuhuri kutoka Uganda na Rwanda.



No comments:

Post a Comment

Pages