HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

October 10, 2013

VIJANA WATAKIWA KUJIUNGA NA MFUKO WA NSSF

Na Mwandishi wetu, Tanga

MWANADADA anayetamba katika tasnia ya muziki wa kizazi kipya nchini, Mwasiti Almas amewataka vijana kujiunga na mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), ili kujihakikishia usalama wa maisha bora kutokana na fursa zilizopo  kwenye mifuko hiyo kwasasa.

Akizungumza juzi katika viwanja vya Tangamano mjini hapa, msanii huyo alisema kwasasa vijana ndio nguvu kazi ya taifinayotegemewa, lakini kukosa uelewa wa kuzitumia fursa zilizopo zimesababisha wengi kuwa tegemezi katika familia zao na mzigo kwa taifa.

“Mtanzania wa kawaida kama unataka mitaji ya uhakika, ingia kwenye mfuko wa NSSF kani mfuko huo umetusaidia sana sisi tumetupa mwangaza mkubwa wa maendeleo,” alisema.
Msanii wa hip hop, Niki wa Pili alisema vijana wengi wamekosa taarifa sahihi kuhusu namna ya kutumia fursa zilizopo katika kujiletea maendeleo yao na taifa kwa ujumla hali inayowafanya waonekane ni tegemezi.

“Tatizo ni jinsi tunavyowaandaa vijana kwani elimu wanayoipata haiendani na mazingira ya fursa yaliyopo kwenye maeneo yao, utaona kijana toka anapata elimu ya msingi hadi chuo hakuna kitu cha ujasiriamali alichojifunza wala taarifa zozote kuhusu kujitegemea alizozipata,” alisema.

 Alisema ifike wakati vijana walioko shuleni wasiishie kupata elimu ya darasani bali waandaliwe kwaajili ya kuhakikisha wanapewa na elimu nyingine ya fursa zilizopo kwenye eneo husika walipo.

Naye Mwakilishi wa NSSF Makao Makuu, Salim Kimaro alisema mfuko huo kwasasa umejikita katika kuwasaidia vijana kiuchumi kwa kuwakopesha mikopo, ambayo wataitumia kuendesha biashara zao walizobuni.

“Chamsingi ni vijana kujiunga katika vikundi na kuanzisha vyama vya akiba na mikopo SACCOS, baada ya hapo wawe mwanachama wa mfuko wetu na wawe wamechangia kwa kipindi cha miezi sita watapata fursa ya kukopeshwa fedha,” alisema Kimaro.


No comments:

Post a Comment

Pages