![]() |
| Mkubwa Fella |
Kwa mujibu wa Mkubwa Fella, licha ya wasanii wengi
kukataa kutoa albamu wakihofia soko lake kuporomoka, atahakikisha albamu ya
Yamoto Band itauza na kurudisha faida.
Alisema kuwa, yeye ndio meneja wa kwanza wa muziki huo
hapa nchini, hivyo kwa kutumia ukongwe huo atatumia akili za ziada ili kugundua
tatizo lilipo na kujitahidi afanye kile anachokusudia.
"Mtu mzima ni mtu mzima tu, mimi nitahakikisha
narehesha soko la albamu, unajua msanii anajiona bora pale anapokuwa na albamu
na hawa wasanii wa Yamoto ni wadogo hivyo natakiwa kuwakuza kimuziki
unaotakiwa, mimi nitalazimisha kuwashawishi hao wadau mpaka soko
litarudi," alisema.
Wasanii walio wengi kwasasa wamesitisha utoaji wa albamu
kutokana na kutokuwepo kwa soko hilo.





No comments:
Post a Comment