HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

May 23, 2015

Bayport yazindua huduma mpya ya mikopo ya viwanja kwa Watanzania wote

 Mkurugenzi wa Bayport Financial Services, John Mbaga, akizungumza jambo katika uzinduzi wa huduma mpya ya mikopo ya viwanja katika mradi wa Vikuruti, Kibaha, mkoani Pwani. Uzinduzi huo ulifanyika Ijumaa ya Mei 22, katika Hoteli ya Serena na kuhudhuriwa na watu mbalimbali, wakiwamo viongozi wa serikali. (Na Mpigapicha Wetu).

Na Mwandishi Wetu

 KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida, taasisi ya Kifedha ya Bayport Financial Services, inayojihusisha na mikopo, imeanzisha huduma mpya ya kukopesha viwanja watumishi wa umma, wafanyakazi wa kampuni za kawaida na wajasiriamali wa aina zote.
  
 Kuanzishwa kwa huduma hiyo mpya kumetokana na taasisi hiyo kupania kuboresha maisha ya Watanzania, likiwamo kundi la wajasiriamali ambalo limeendelea kusahauliwa na kampuni nyingi kupewa mikopo.


 Akizungumza mwishoni mwa wiki katika uzinduzi huo uliofanyika katika Hoteli ya Serena, Mkurugenzi wa Bayport Financial Services, John Mbaga, ni kusudio lao kutoa fursa ya watumishi wa umma, wafanyakazi wa kampuni na wajasiriamali wakipata nafasi ya kutimiza
 ndoto za kumiliki ardhi nchini Tanzania.


 “Huduma yetu katika mradi wa Vikuruti, Kibaha, mkoani Pwani, fomu zake zinapatikana katika matawi yote ya Tanzania Bara, huku fomu za kukopeshwa viwanja hivyo zikipatikana kwa wiki mbili, kuanzia Mei 22 hadi Juni 10 mwaka huu.

 “Si lazima uwe mtumishi wa umma ili uwe na sifa ya kukopeshwa viwanja, ila hata wajasiriamali nao wamekumbukwa katika huduma hii nzuri kwa Watanzania wote, hivyo ni wakati wao sasa kuiunga mkono taasisi hii ili iweze kuwakomboa na kuwakwamua pia,’ alisema Mbaga.

 Akimwakilisha Mkuu wa wilaya ya Kibaha katika uzinduzi huo, Afisa Mipango wa wilaya hiyo, Obed Katonge, alisema kwamba Bayport imebuni huduma nzuri inayofaa kuungwa mkono na Watanzania wote, hasa kwa kuingia kwenye sekta ya ardhi inayopanda thamani siku hadi siku duniani kote.


 “Serikali hususan kwenye wilaya yetu ya Kibaha tumepokea huduma hii kwa mikono miwili, ukizingatia kuwa wilaya yetu ni kati ya maeneo yanayokuwa kwa kasi, hivyo tunaamini tutaendelea kushirikiana na Bayport kwa ajili ya kuwapatia mwangaza wateja na wananchi wote kwa ujumla,” alisema Katonge.


 Naye Meneja Masoko na Mawasiliano wa Bayport Financial Services, Ngula Cheyo, alisema kuanzishwa kwa huduma hiyo mpya ni njia ya kunapanua wigo wao na shabaha ya kuwafaidisha wateja wao na Watanzania wote kwa huduma na bidhaa zilizothibitishwa kwa ubora zaidi.


 “Bayport ilikaa na kufanya tafiti kadhaa zenye nia ya kujenga jamii na kuinua uchumi wa Watanzania wote, hivyo tukaona ipo haja ya kufungua ukurasa huu wa kukopesha viwanja, huku wateja wetu wakitakiwa kulipa kila mwezi katika vipindi vya miezi
 24, ambapo kiwanja cha chini kabisa kinapatikana kwa Sh 1,700,000 na nzuri zaidi wateja wetu wanaweza kuona huduma nyingine nzuri za mikopo kwa kupitia tovuti yetu yawww.kopabayport.co.tz ,” alisema Cheyo.


 Naye Meneja Bidhaa wa Bayport Financial Services, Thabit Mndeme, alisema makato ya kiwanja chenye thamani ya Sh 1,400,000 kwa mjasiriamali ni 105,181.55, wakati mtumishi wa umma akilazimika kukatwa Sh 73,684.49, huku akiongeza kuwa mtu anaweza kupata kiwanja kwa malipo ya fedha taslimu.


  “Naomba Watanzania wajitokeze kwa wingi kukopeshwa viwanja hivi ili watimize ndoto zao za ujenzi wa nyumba, maana Bayport imekuja kwa ajili ya kuboresha maisha ya Watanzania wote, maana tangu sasa kila mtu anaweza kuwa baba au mama mwenye nyumba,” alisema Cheyo.


 Mbali na huduma ya mkopo wa viwanja, Bayport pia inatoa mikopo mbalimbali ya bidhaa, mikopo ya fedha taslimu, bima ya elimu kwa uwapendao, huku mikopo yote hiyo ikiweza kupatikana kwa njia ya mtadao wa www.kopabayport.co.tz.

No comments:

Post a Comment

Pages