HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 04, 2015

MKUBWA FELLA AWAITA MASHABIKI ESCAPE ONE

NA ELIZABETH JOHN





MKURUGENZI wa bendi ya Yamoto, yenye maskani yake Temeke jijini Dar es Salaam, Said Fella ‘Mkubwa Fella’ amewataka Watanzania kujitokeza kwa wingi katika ukumbi wa Escape One Mikocheni kuwaunga mkono wasanii wa bendi hiyo katika uzinduzi wa ngoma yao mpya.

Uzindizi wa ngoma yao mpya ya ‘Cheza Kimadoido’ unatarajiwa kufanyika Jumamosi katika ukumbi huo huku kiingilio kikiwa ni shilingi 10,000.

Kwa mujibu wa Mkubwa Fella, wasanii ambao watasindikiza uzinduzi huo ni bendi ya Mapacha Watatu, Tunda Man, Madee, Chege na Temba.

“Tunatakiwa kuwasapoti vijana wetu ili muziki wetu uendelee kukua, pia tunashukuru kwa kuipokea ngoma hii kwa mikono miwili tunaomba tuendelee kupeana sapoti kazika soko la muziki wetu,” alisema.

Bendi hiyo ambayo inafanya vizuri katika soko la muziki huo, inaundwa na wasanii wanne ambao ni Aslay, Maromboso, Beka One na Enock Bella.



No comments:

Post a Comment

Pages