HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 04, 2015

RUBBY AWAPA NAFASI MASHABIKI KUIJADILI VIDEO YA 'NA YULE'

NA ELIZABETH JOHN


CHIPUKIZI wa muziki wa kizazi kipya nchini, kutoka Nyumba ya Kukuza vipaji Tanzania (THT), Rubby amewapa nafasi wapenzi wa kazi yake kuitathimini video ya wimbo wake wa ‘Na Yule’ ambao ameusambaza juzi katika vituo mbalimbali vya televisheni.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Rubby alisema kuwa, kazi hiyo anaamini itafanya vizuri kutokana na mazingira ambayo ametumia kuitengenezea.

“Nina amini nimefanya kazi nzuri, ila kwa sababu nina mashabiki ambao wanafatilia muziki wangu nitaomba wanipe maono yao katika kazi hii ili nijifunze na nisikirudie katika kazi nyingine,” alisema.

Alisema kuwa anaomba wapenzi zake waendelee kumpa sapoti katika kazi zake ambazo zinakuja kwani kuna kazi nyingi ambazo anatarajia kuzisambaza.

Rubby ametamba katika soko la muziki huo kutokana na kusambaza ngoma yake ya ‘Na Yule’ ambayo imefanya vizuri sokoni kutokana na ujumbe uliopo ndani yake.

No comments:

Post a Comment

Pages