HABARI MSETO (HEADER)


August 09, 2016

Chama Cha Kuogelea kinahitaji Milioni 71 kwa ajili ya mashindano ya Dunia Desemba Canada

Na Mwandishi Wetu
 
Chama Cha kuogelea Tanzania (TSA), kinahitaji dola za Kimarekani 32,500 (Sh 71 milioni) kwa ajili ya kuipeleka waogeleaji nane (8) wa timu ya Taifa kwenye mashindano ya Dunia yaliyopangwa kufanyika mjini Windsor, nchini Canada.
 
Katibu Mkuu wa TSA, Ramadhan Namkoveka alisema kuwa timu ya Taifa ya Tanzania inakuwa na jumla wachezaji 11 ambapo kati ya hao, wachezaji watatu watalipiwa na Shirikisho la Mchezo wa kuogelea duniani (Fina).
 
Namkoveka  alisema kuwa kila muogeleaji anatakiwa kulipiwa ni dola za Kimarekani 4,100 (Sh 8.2 million). Alisema kuwa TSA kwa sasa haina fedha za kuweza kuwapeleka wachezaji wote hao kwa ajili ya mashindano hayo.
 
 Kwa mujibu wa Namkoveka, gharama kubwa kuipeleka timu  na kuwaomba wadau wa mchezo huo kuwasaidia ili kuweza kufanikisha lengo lao ka kuipeleka timu hiyo katika mashindano hayo.
 
“Tunahitaji kupeleka waogeleaji wengi zaidi katika mashindano haya ambayo ni makubwa duniani, mchezo wetu unakuwa kwa kasi na tunahitaji kupata waogeleaji wenye uzoefu katika mashindano ya kimataifa,” alisema Namkoveka.
 
Alisema kuwa TSA kimeunda kamati ya watu… kwa ajili ya kutafuta fedha kwa ajili ya kuhakikisha timu hiyo inakwenda kwenye mashindano hayo. 
 
 Alisema kamati hiyo unaundwa na Mkurugenzi wa Fedha wa TSA, Phillip Saliboko, Asma Hilal, Amina Mfaume (Mkurugenzi wa Ufundi wa TSA), Inviolata Itatiro (Katibu Mkuu wa klabu ya Dar Swim Club),  Geetha Prashant , Hamisi Mhini na Katibu Mkuu wa klabu ya Dar es Salaam Swim Club (DSC), Inviolata Itatiro.
 
Wachezaji waliochaguliwa kuunga timu hiyo ya Taifa ni Hilal Hilal, Aliasghar Karimjee, Ammaar Ghadiyali, Denis Mhini, Adil Bharmal, Joseph Sumari  ambao watashiriki kwa upande wa wanaume na kwa upande wa wanawake ni Catherine Mason, Sylvia Caroiao, Sonia Tumiotto, Mariam Foum na  Magdalena Moshi.

No comments:

Post a Comment

Pages