Mashabiki wa Lipuli FC wakishangilia timu yao baada ya kuifunga Yanga bao 2-0 katika mchezo wa nusu fainali ya kombe la Azam Sports Federation Cup (ASFC) katika mchezo uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Samora mjini Iringa. (Picha na Tullo Chambo).
NA MWANDISHI WETU, IRINGA
WANA
Paluhengo Lipuli FC, wamekatiza ndoto za Yanga kuwania tiketi za kuiwakilisha
nchi Tanzania katika Kombe la Shirikisho Afrika (CAF CC), baada ya kuwachapa
mabao 2-0, katika nusu fainali Kombe la Shirikisho la Azam Sports (ASFC).
Hii
ni mara ya pili kwa Lipuli kuifyatua Yanga katika Uwanja wa Samora mjini hapa
mwaka huu, baada ya Machi 16, kuzaibua bao 1-0, lililofungwa na Haruna Shamte,
katika pambano la Ligi Kuu Tanzania Bara (TPL).
Wabishi
hao Iringa, walitinga fainali ya ASFC baada ya kuibuka na ushindi huo kwenye
Uwanja wa Samora mjini hapa, na sasa wanaenda kuumana na Azam FC katika fainali
kali kwenye Uwanja wa Ilulu mjini Lindi, hapo Juni 2.
Katika
mchezo huo uliochezeshwa na mwamuzi Shomary Lawi wa Kigoma, mabao ya Lipuli
yalifungwa na mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Paul Nonga dakika ya 27 na
Daruwesh Saliboko dakika ya 38, na kudumu hadi filimbi ya mwisho.
Mchezo
huo ambao uliohudhuriwa na maelfu ya mashabiki kutoka ndani na nje ya mkoa wa
Iringa, Yanga iliuanza mpira kwa kasi na kukosa nafasi za kufunga mabao, lakini
safu yao ya ushambuliaji ilikuwa butu.
Licha
ya mwanzo huo wa Yanga, Lipuli walicheza kwa umakini na kufanikiwa kupata bao
la kwanza dakika ya 27 kupitia kwa Nonga ambaye alimaliza mpira uliotemwa na
kipa wa Yanga, Klaus Kindoki, kufuatia shuti kali la Saliboko.
Kuingia
kwa bao hilo, kuliiongezea nguvu Lipuli, ambao walicharuka na kufanikiwa kupata
bao la pili dakika ya 37, likifungwa Saliboko, akitumia vema makosa ya Kindoki
ya kuutema mpira alioanza kupiga yeye mwenyewe na kuukwamisha nyavuni.
Licha
kufanya mabadiliko mbalimbali kwa timu zote mbili, lakini hayakuleta tija na
Lipuli iliyokuwa chini ya Kocha, Samwel Moja na Suleiman Matola waliibuka na
ushindi wa mabao 2-0 na kutinga fainali.
Kwa
matokeo hayo, Yanga inaelekea kuwa mtazamaji wa michuano ya klabu Afrika msimu
ujao, kwani licha ya kuongoza msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara (TPL), wana
nafasi finyu ya kuwapoka mahasimu wao Simba taji hilo wanalolishikilia.
Na
kipigo hiki kinakuja siku mbili baada ya kuchaguliwa kwa uongozi mpya wa klabu
chini ya Mwenyekiti, Dk. Mshindo Msolla na Makamu Mwenyekiti, Frederick
Mwakalebela, waliochaguliwa juzi katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika Bwalo la
Maofisa wa Pilisi, Oysterbay, Dar.
Katika
uchaguzi huo, wagombea waliochaguliwa katika nafasi ya Wajumbe wa Kamati ya
Utendaji ni Hamad Islam, Mhandisi Bahati Mwaseba, Dominick Ikute, Kamugisha
Kalokola, Arafat Haji, Salum Ruvila, Saad Khimji na Rodgers Gumbo.
Akizungumzia
mchezo huo, Kocha Msaidizi wa Lipuli FC, Matola alisema anashukuru vijana wake
wamefanya kile walichokuwa wamepanga, ambacho ni kucheza fainali ASFC ilikusaka
tiketi ya kucheza kimataifa.
Alisema
fainali hiyo dhidi ya Azam FC itakuwa ngumu kutokana na ubora waliokuwa nao,
lakini wanafungika, na kwamba wataenda Lindi kushinda mechi hiyo.
Kwa
upande wake, Kocha wa Yanga, Mwinyi Zahera alisema kipindi cha kwanza beki yake
ilicheza ovyo ndio maana wameadhibiwa.
Alisema
kwa walipofika wanashukuru kwani msimu huu hawakuwa na malengo ya kufanya
vizuri katika Ligi Kuu wala Kombe la Shirikisho ASFC.
Baada
ya kumalizika kwa mchezo huo, uwanjani liliibuka shangwe kwa mashabiki
wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mjini, Richard Kasesela, huku milio ya
woh! woh! Who ikianikiza, wakiigiza kama Mbwa.
Kikosi
cha Lipuli FC kilikuwa; Yusuph Mohammed, Haruna Shamte, Paul Ngalema, William
Lucian ‘Gallas’, Ally Sonso, Freddy Tangalu, Miraj Athumani ‘Madenge’/Novaty
Lufunga, Jimmy Shoji, Paul Nonga, Dariwesh Saliboko na Zawadi Mauya/Steven
Maganga.
Yanga
SC; Klaus Kindoki, Paul Godfrey, Mwinyi Hajji/Kelvin Yondani, Abdallah Shaibu
‘Ninja’, Andrew Vicent ‘Dante’, Feisal Salum, Mrisho Ngassa, Mohammed Issa
‘Banka’/Amissi Tambwe, Heritier Makambo, Papy Tshishimbi na Ibrahim Ajib/Juma
Abdul.
No comments:
Post a Comment