HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

September 06, 2019

TMA yatangaza upepo mkali

NA IRENE MARK

MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), imetoa tahadhari ya upepo mkali na mawimbi makubwa baharini kwa siku tatu mfululizo kuanzia kesho, Septemba 7,2019.

Tahadhari hiyo imetolewa leo na ofisi ya uhusiano ya mamlaka hiyo ikitaja baadhi ya maeneo ya mikoa ya ukanda wote wa Pwani, Lindi, Mtwara, Dar es Salaam, Tanga, maeneo ya Ziwa Nyasa na visiwa vya Unguja na Pemba.

Kwa mujibu wa kifurushi cha siku tano cha tahadhari za hali ya hewa, TMA imewashauri watumiaji wa tarifa zao kuchukua hatua ili kudhibiti maafa yanayoweza kujitokeza.

No comments:

Post a Comment

Pages