Maendeleo yanakuja na mambo mengi mazuri, mfano hapo awali
ili kuwasiliana na ndugu zako mkoa mwingine ilikuwa ni lazima usafiri, au
uandike barua na uende kilomita kadhaa udumbukize kwenye sanduku la posta na
posta waisafirishe pengine wiki mbili ndipo ifike kule inapokwenda, mpaka
ujibiwe miezi kadhaa inakuwa imepita.
Taarifa kama misiba kwa watu walio mbali walikuwa wanazipata muda mrefu baada
ya mazishi, redio ilikuwa moja tu, Redio Tanzania huu ni mfano tu. Taasisi za
fedha zilikuwa chache sana, benki
ilibidi ujaze karatasi nyingi, faili lako litafutwe uli kutambua sura na saini
yako.
Foleni zilikuwa ndefu sana, kwenda benki ilikuwa ni shughuli ambayo
lazima uitengee muda tena wa kutosha. Kwa kifupi teknolojia kwenye Nyanja nyingi hiyo ilikuwa
duni sana.
Mabadiliko ya teknologia na ukuwaji wa uchumi ukihuishwa na
elimu pana umeleta mapinduzi makubwa sana katika jinsi ambazo tunaweka pesa
zetu, leo sio lazima uende benki kuchukuwa au kuweka pesa zako, kwa njia ya
simu au kadi unaweza kuchukuwa pesa zako bila kuongea na mtu, yaani mashine tu
na kutumia alama mbali mbali kama vidole, nywila, mashine inakupa hela huhitaji
kuongea na muhudumu au meneja wa benki, na miamala hii unaweza ifanya kijijini
na hata mjini, na popote pale duniani.
Katika Nyanja ya uwekezaji unaweza weka akiba kwa simu yako,
ukaitumia kama daraja la kukuwezesha kuwekeza, mfano ukachukuwa pesa ukaweka
kwa akaunti yako ya akiba benki au ukachukuwa pesa ukawekeza kwenye akaunti
yako ya uwekezaji ya UTT AMIS, kwa simu unaweza ukakata bima yako ya afya,
unaweza ukanunua piki piki kwa simu hiyo
hiyo na makusanyo ya kila siku ukayawekeza
kila siku kwa simu. Yaani kwa kifupi kukua kwa tekinolojia kuna rahisisha
maisha.
Urahisi huu una faida na hasara zake. Wakati faida ni kama
vile kuokoa muda, uharaka wa miamala, usalama wa miamala, na kuongeza mzunguko
wa fedha kwenye uchumi jambo ambalo ni la kheri hasara zipo pia kama vile
gharama zaidi, kupata ujumbe kutoka kwa matapeli, kupoza simu, na kama nywila
yako ikaangukia kwenye mikono mibaya.


Baada ya kuunganisha simu yako na akaunti yako ya
benki,tayari utakuwa unaweza kufanya miamala, kuna tofauti kubwa sana pale
unapokuwa umeishika noti/hela mkononi na kuihesabu ili kufanya malipo fulani.
Kwanza ukiishika unaiskia yaani kuna mgusano kati ya mwili wako na hela halisi,
unapolipa inatoka mkononi mwako unaiona inapokelewa upande ule unapo lipia
bidhaa au huduma fulani na unaona ikipokelewa.
Wakati wa kulipa unahesabu na
ukilipa ndoa yako na pesa hiyo imekwisha sababu unaona vile inakwenda roho
inakuuma, na inaweza kukufanya ujiulize mara nyingi ni lazima nivunje hii ndoa,
mbona nalipa sana na maswali mengine mengi.
Lakini kama unatumia simu kulipa au kadi –tunasema kama una
chanja hela huioni, uhusiano wako na hiyo hela unakuwa kama uko mbali sana.unakuwa
kama vile si wa moja kwa moja. Wakati mwingine haikupi uchungu kwa sababu
hakuna mgusano, huioni, ina katwa huko kwa huko, na pengine mpaka uchukuwe
taarifa yako ya pesa kutoka benki au
kutoka kampuni ya simu ndipo una stuka kuwa ulifanya miamala ya gharama kubwa
sana, na hapo ndipo ambapo kama hukua makini roho inakuuma, macho yanakutoka.
Kukosekana kwa msuguano kati ya mkono wako na hela kumekufanya usijisikie kama huja
tumia hela kumbe umetumia tena sana tu.
Swali kubwa la kujiuliza ni wapi nilipe kwa pesa halisia na
ni wapi nilipe kwa kutumia simu au kadi za benki na hii itanisaidia vipi
kutunza pesa zangu kwa jili ya kuwekeza?
Ukweli ni kuwa ukitembea na hela unaweza kuzipoteza, pochi
inaweza ibwa, potea,, kadi na simu pia
zinaweza kupotea lakini mtu aki okota
mathalani ni lazima awe na nywila (password), kwa maana nyingine utakuwa
umepoteza simu au kadi ila si pesa.
Kama unataka kuwa mwekezaji ni lazima ujipema kama kwa
kutumia simu au kadi za malipo huikupelekei kuwa na ki-here here cha kutumia
pesa hovyo. Unalo jukumu la kuhakikisha kuwa matumizi yako yanakwenda sambamba
na bajeti yako.
Katika tafiti za matumizi kwa njia ya simu au kadi
inasemekana kuwa watu hutumia asilimia 23% zaidi ikilinganishwa na kama
ingekuwa wanalipa kwa pesa moja kwa moja. Hii tukiweka kwa tarakimu ni kuwa kwa
kila shilingi 100,000 kuna shilingi 23,000 ambazo ungeziokoa. Ina maana kwa
kila milioni ungeokoa shilingi 230,000 na hii kama ni kwa mwezi ina maana kwa
mwaka inakuwa shilingi 2,760,000 kwa miaka 10 matumizi haya ambayo si ya muhimu
yanaweza kuwa zaidi ya shilingi 27,600,000.
Kwa mtu makini na mwenye kujuwa kuwekeza angewekeza hizo
shilingi 230,000 kwa mwezi ambazo amekuwa akizitumia vibaya kwa riba ya asilimia 12 kwa miaka hiyo kumi
angeweza kupata shilingi 52,908,898.98
Uwekezaji wa namna hii unawezekana kupitia mifuko ya
uwekezaji wa pamoja ya UTT AMIS, kwa mfano huu ina maana miaka 10 umepoteza
shilingi 27,600,000 ambayo ungeiwekeza kupitia mifuko ya UTT AMIS ingekupa
shilingi 52,908,898.98. Tafiti zinaonyesha kua kuna watu hutumia mpaka aslimia
30 kwa kutokuwa makini na tekinoljia hizi za kisasa. Na pia ukumbuke kadri
kipatao chako kinavyokukuwa ndivyo kiasi unachopoteza kinazidi kuwa kikubwa.
Kuumbuka kulipa kwa njia za simu au kadi si vibaya, hizi
namna hazina ubaya wowote ule, mbaya ni wewe mtumiaji wa hizo namna.
Unachotakiwa kukumbuka ni kila unapotumia kadi au simu ni kma vile umelipa pesa
kwa mkono wako kutoka mfukoni kwako yaani ni lazima hiyo njia ya malipo uiweke
kwenye maana halisi ya malipo. Ni lazima utafsiri uchungu au furaha ambayo
ungepata kwa kulipa ‘cash’.
Uwekezaji wa pamojakpitia UTT AMIS
ni daraja zuri sana la kuwekeza, kwani ni rahisi na unapata nafasi ya kuwekeza
pesa ndogo ndogo ambazo pengine ungezitumia vibaya, watu wengi wanachanga pesa
zao katika mfuko mmoja na kumpa meneja (UTT AMIS) ambaye anaziwekeza pesa hizo
kwa kuzingatia waraka wa makubaliono, anaziwekeza kwa ufanisi, huku akizingatia
usalama, uwazi na taratibu zote kwa malengo ya kuzipa pesa hizo thamani zaidi.
Jambo zuri kuhusu uwekeza wa pamoja ni huhitaji kuwa na pesa nyingi ili uwe
mwekezaji anzia shilingi 10,000 tu unaweza kuwa mwekezaji hii shilingi 10,000
inaweza kua ile ambayo ungeiteketeza kwa kutumia vibaya au ile uliyo jilipa
kwanza yaani ile ambayo ulitenga baada ya kupata kipato fulani ukaitenga kwa
ajili ya maisha ya baadae na kuiwekeza na ukafanya hivyo mara kwa mara.
Na
uzuri unaweza kuwekeza kwa simu au kwa kwenda benki ya CRDB na kuweka pesa zako
kwenye akaunti yako ya UTT AMIS.
Ili kuwa mwekezaji ni lazima
ujisome ujuwe mambo yanayo kuchochea kutumia pesa. Mara nyingi matumizi
yanendana na tabia, watu na jamaa iliyo kuzunguka, mtazamo, na pengeni vile
mwili unajisikia-tamaa. Kikubwa hapa ni kuangalia pesa unayoweza kutenga kutoka
kwenye kipato chako, pesa unayoweza kupata bila kutegemea na kuepuka yale mambo
yanayo kufanya utumie pesa vibaya, ili pesa hizo uweze kuzipa thamani zaidi kwa
kuwekeza sehemu zenye tija kama vile UTT AMIS.
Kama kuna mazingira ambapo kuwepo
kwako pale kunakufanya utumie zaidi ya epuke. Kwa mfano ukiwa baa kama baada ya
bia moja au mbili unaanza kunua hovyo hovyo, na malengo yako ni bia mbili basi
kunywa nyumbani. Au kama starehe yako ni kuwa baa basi chukuwa pesa ya bia
mbili tu. Hii itakusaidia kuokoa hela kwa ajili ya mambo muhimu kama vile
kuwekeza kwa ajili muda wa kustaafu.
Wengine wakiwa na hasira wana
kwenda kulewa, badala ya kwenda kulewa vaa raba tembea kilomita mbili mpaka
tatu, msongo wa hasira utapungua. Na bado utakuwa umeokoa pesa.
Je ukiwa na bibi au bwana yako unatumia
zaidi? Pia ukiwa na marafiki fulani matumizi yako yanongezeka? Marafiki wazuri
wanaweza kuwa wabaya pia hususani kama ni vinara wa matumizi. Badala ya
kukutana nao sehemu za gharama, kutana nao kwenye baa au migahawa ya bei ndogo.
Kumbuka soda coca cola ni hiyo hiyo lakini bei yake hutofautiana kati ya hoteli
na hoteli, dukani ni shilingi 600 lakini kwenye hoteli kubwa ni shilingi
2500.
Je una staili gani ya maisha? Tumia
kulingana na mfuko wako, ukiona matumizi yako yanazidi kile kilichopo mfukoni
mwako tambua hutaweza kuwa mwekezaji, kuna watu wanapenda maisha ya juu sana.
Unachukuwa mkopo wa milioni 20 unaenda nunua gari la pesa yote hiyo ili
uonekane?? Mwekezaji atanunua piki piki au gari isiyozidi hata milioni 10,
kiasi kilicho baki atawekeza, Badilika acha sifa.
Ili usitoke nje bajeti, hakikisha
unafuatilia matumizi yako ikibidi andika matumizi. Hii itakusaidia kufahamu
kila shilingi umeitumia vipi. Na kuweza kufanya tathimini ya ni wapi ungetumia
vizui zaidi na ni wapi umekosea. Pia itakusaidia kujuwa pesa zako nyingi
zinakwenda kwenye matumizi gani zaidi. Ukiweza kuepusha shilingi 3,000 kwa siku
inakuwa shilingi 90,000 kwa mwezi, hizi ni pesa nyingi sana kwa mwaka na ni
pesa nyingi kwenye uwekezaji wa pamoja katika miaka ya baadae.
Pendelea
kulipa kwa keshi badala ya kadi kama Makala hii ilivyo ainisha hapo mwazo.
Mambo mengine ya kufanya ni kama vile kupanga malengo ya muda mfupi na yanyo
fikika unarekebisha malengo kabla unavyo yamudu. Usiweke malengo ambayo yako
nje ya uwezo wako. Jifunze jinsi ya kubajeti sababu bajeti ndiyo njia ya
kukupeleka kwenye Uhuru wa Pesa.
KUmbuka kwenye kutumia kuna vitu
muhimu, kuna dharura na kuna vitu unavipenda. Mapenzi yasizidi vitu au maswala
muhimu, jambo muhimu ni kuwekeza kwa ajili ya kesho yako, kurahisisha maisha
zaidi.
Kumbuka si rahisi kutokuwa na
madeni, weka mpango wa kulipa madeni yako. Kumbuka madeni yenye riba ni hatari
sana kwani muda unavyokuwa mrefu ndivyo mzigo unakuwa zaidi. Mikopo inatakiwa
iwe ni kwa ajili ya kufanya maisha yawe bora na si kuyanya yawe magumu au mzigo
usio bebeka.
Ki ujumla kuna faida nyingi sana
kiuchumi kwa kutumia simu kama chombo cha kufanya miamala, utalipia mahitaji
yako sokoni, dukani n ahata hosipitali, Utalipia bili za maji, umeme,
kodo za nyumba, viwanja, bima na mabo kadha wa kadha. Kulipa
kwa simu ni rahisi na haraka, na pia salama kwa kiwango kikubwa sana. Ukiwa na
simu si lazima uwe na akaunti ya benki hiyo hiyi simu yaweza kuwa sehemu ya
kuhifadhi pesa zako. Makala hii ilijaribu kukupa jicho la ziada pia tujaribu
kuwangalia faida hizo na hasara zake ukilenga dhana nzima ya uwekezaji kwa pamoja.
No comments:
Post a Comment