HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

May 12, 2021

Wandishi wanakumbwa na vitisho na manyanyaso kazini

 


Jaji mstaafu Justice Makaramba.

 

 

NA HAMIDA RAMADHANI

 

 

JAJI Mstaafu Justice Makaramba amesema, wanahabari wengi wamekuwa wakikumbwa na vitisho na manyanyaso pindi wanapokuwa katika majukumu ya kila siku kazini.

 

Pia, amesema kumekuwa na kasumba nyingine ya waandishi wa habari kesi zao kutofatiliwa mahakamani kwa dhana ya  kuwashitaki watu wasio julikana.

 

Amebainisha hayo leo Jumatano, tarehe 12 Mei 2021 na Jaji Makaramba wakati akiwasilisha mada ya mifumo ya kikanda na kimataifa ya kuhakikisha usalama wa wanahabari katika mafunzo yalioandaliwa na Mtandao wa Utetezi wa haki za binadamu Tanzania THRDC Mkoani Morogoro.

 

Aidha ameyataja matukio mabaya yanayowakumba waandishi kuwa ni pamoja na kuuawa, kutekwanyara, kupotea, kuwekea kizuizini huku akisisitiza matukio hayo huwakumba waandishi wanaoandika habari hususan za uchunguzi au kuigusa hasa serikali.

 

Hata hivyo, amesema kwa Mujibu wa Takwimu ilizotolewa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), zinasema kuanzia mwaka 2018 mpaka 2019 kulikuwa na matukio 156 ya kuuawa kwa waandishi duniani.

 

"Hii inamaanisha kila ndani ya siku nne, mauaji ya mwandishi yanatokea na mauaji mengi yamekuwa yakitokea  kwenye nchi ambazo hazina vita, nchi ambazo zimejaa na amani na utulivu wa kutosha," amesema Jaji Mstaafu Makaramba.

 

Jaji huyo amesema, kazi ya mwandishi ni pamoja na kuihabarisha jamii kuhusu masuala mbalimbali.

 

SABABU 3 ZA KWANINI WAANDISHI KUWA SALAMA.

 

Jiji Mkaramba amezitaja kuwa

1:  Ili aweze kufanya kazi yake kwa weledi,

2: Tasnia ya habari isiwe hatarini, waandishi wa habari wakiuawa na Watu wasiadhibiwe kila mtu atogopa kuwa mwanahabari

3: Wasijulikane, kwani kunaweza kuwaweka katika hatari.

 

Hata hivyo, amesema ili kuzuia majanga hatari yanayowakumba waandishi, ni pamoja na kuwepo kwa mifumo ya kudai haki za binadamu kuanzia ngazi ya Kimataifa na Kikanda ili haki za waandishi wa habari ziweze kupatikana.

 

 

No comments:

Post a Comment

Pages