HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

July 10, 2021

Wanaosomea umeme watakiwa kutembelea banda la chuo cha uwalimu MVTTC

 Na Asha Mwakyonde, Da es Salaam


WANAFUNZI wanaosoma umeme wametakiwa kujitokeza kwenye viwanya vya kimataifa vya mwalimu nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa ambapo maonyesho ya kimataifa ya 45 ya sabasaba yanafanyika na kutembelea kwenye banda la chuo cha uwalimu cha mafunzo ya ufundi stadi MVTTC EETAMOROGORO) ili kupata elimu  kuhusu umeme.

Akizungumza na waandishi wa habari jana kwenye viwanja hivyo vya maonyesho  wilayani temeke Frank Urio ambaye ni mhandis kutoka chuo hicho kilichopo mkoani Morogoro alisema kuwa wapo katika maonyesho hayo na wamekuja na kifaa kipya kuhusu umeme.

 Amesema kuwa kuna changamoto kubwa sana  kwa wanafunzi ambao wanakwenda kufanya mafunzo kwa vitendo na ndio maana kupitia maonyesho hayo wamekuja na  kifaa ili kuweza kuwapa elimu stahiki na kifaa hicho ni teknolojia mpya na ndani yake kuna  mafunzo ya aina mbili ambayo ni electronic mashine nanyingine.

 “Ndugu waandishi kikubwa kupitia maonyesho haya tunawaomba wanafunzi waje ,na wajitokeze kwa wingi ili waje kupata elimu stahiki kuhusu  umeme na kama mnvyojua changamoto za umeme  kwahiyo tupo hapa hadi julai 13  hivyo wajitokeze.”amesema mhandisi Urio

 Ametoa wito kwa wanafuzni ambao wamesoma umeme waje ili wafundishwe kujua namna ya kuona vifaa hivyo jinsi vinavyo kufanya kazi ili akiwa katika maeneo yake yakazi asikutane na changamoto kubwa.

 Naye Sophia Tuka ambaye ni mkufunzi mwandamizi chuoni hapo akizungumzia kozi ambazo zinatolewa chuoni  hapo hususani mwaka huu wa masomo alisema kuwa chuo hicho kinatoa kozi mbalimbali za ualimu na wanaandaa walimu wanaofundisha ufundi.

 Amesema katika chuo chao wanatoa elimu ya ufundi katika ngazi ya cheti na pia wanatoa mafuzo kwa ngazi ya astashahada (Diploma) na mwezi wa tisa masomo yanaaza hivyo  wanafunzi wajitokeze na kujiunga ili kuweza kupata elimu ya ufundi

No comments:

Post a Comment

Pages