HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

August 02, 2021

Wakandarasi wanawake washauriwa kuzingatia nidhamu ya fedha


Kaimu Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS), Mkoa wa Mwanza Mhandisi Vedastus Maribe akifungua rasmi mafunzo ya wakandarasi wanawake wanaotumia teknolojia stahiki ya nguvu kazi katika utengenezaji wa barabara jijini Mwanza.

Sehemu ya wakandarasi wanawake wanaotumia teknolojia stahiki ya nguvu kazi katika utengenezaji barabara wakiwa katika mafunzo hayo yaliyofanyika jijini Mwanza.



Na Mwandishi Wetu

IMEELEZWA  kuwa kampuni nyingi za wakandarasi wanawake wanaotengeneza barabara kwa kutumia teknolojia stahiki ya nguvu kazi zitafanikiwa endapo wakandarasi hao watakuwa na nidhamu ya matumizi  ya fedha.

Hayo yamesemwa na Kaimu Meneja wa Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS) Mkoa wa Mwanza, Mhandisi Vedastus Maribe wakati akifungua mafunzo wakandarasi wa barabara kwa kutumia teknolojia stahiki jijini Mwanza.

Mhandisi Maribe amewaasa wakandarasi hao kujielimisha vya kutosha kabla ya kuomba kazi ujenzi na ukarabati wa miradi ili wapate faida na kukuza kampuni zao.

"Jazeni vizuri zabuni kwa kuzingatia ukubwa wa kazi, imarisheni usimamizi ili kazi zikamilike kwa wakati, malengo yatimie na kujikomboa kiuchumi," Mhandisi Maribe.

Amehimiza wakandarasi hao kujisajili ili wapewe miradi mingi na hivyo kukua toka wakandarasi wadogo hadi wakubwa.

Naye Mratibu wa Mafunzo hayo Mhandisi Liberatha Alphonce amewataka wakandarasi hao kuongeza mtandao wa wadau ili kubadilishana uzoefu, ujuzi na fursa.

Alisema Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi ina imani na kazi zinazofanywa na wanawake hivyo itaendelea kuwajengea uwezo na kuwapa miradi mingi kutokana na bidii zao.

Zaidi ya wakandarasi wanawake 80, toka mikoa ya Mwanza, Simiyu, Mara, Geita na Kagera wanashiriki mafunzo hayo ambayo pamoja na mambo mengine yatawajengea uwezo katika ujazaji wa zabuni, taratibu za kusajili kampuni, sheria ya manunuzi, namna ya kutumia mfumo wa manunuzi (TANePS) na usimamizi wa mikataba. 

No comments:

Post a Comment

Pages