Waziri wa Nchi Afisi ya Rais, Fedha na Mipango, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Jamal Kassim Ali (kushoto), alipotembelea katika banda la Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) wakati wa Maonesho ya Wiki ya Huduma za Fedha kitaifa yanayoendelea katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam ambapo NSSF inaendelea kutoa elimu ya hifadhi ya jamii kwa sekta binafsi na sekta isiyo rasmi.
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Masha Mshomba akipata maelezo kutoka kwa Afisa matekelezo Mwandamizi Hawa Godigodi, alipotembelea banda la NSSF wakati wa Maonesho ya Wiki ya Huduma za Fedha kitaifa.
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) Masha Mshomba akielezea huduma mbalimbali zinazotelewa na NSSF katika maadhimisho ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa. Katika maadhimisho hayo NSSF inatoa elimu kuhusu hifadhi ya jamii, elimu kuhusu umuhimu wakujiwekea akiba, elimu ya huduma zinazotolewa kwa njia ya mtandao ambapo ndio kipaumbele muhimu cha Mfuko pamoja na kueleza fursa za uwekezaji.
Mkurugenzi wa Idara ya Hifadhi ya Jamii, Ofisi ya Waziri Mkuu, Festo Fute (katikati) akisisitiza jambo alipotembelea banda la Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) wakati wa Maonesho ya Wiki ya Huduma za Fedha kitaifa katika viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam, kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Masha Mshomba, kulia ni Meneja Uhusiano na Elimu kwa Umma, Lulu Mengele pamoja na wafanyakazi wa NSSF.
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) Dkt. John Mduma (kulia), akipata maelezo mbalimbali kuhusu ushiriki wa NSSF katika Maonesho ya Wiki ya Huduma za Fedha kitaifa. Maonesho hayo yanaendelea katika viwanja vya Mnazi mmoja, jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Masha Mshomba akitoa maelezo kwa Waziri wa Nchi Afisi ya Rais, Fedha na Mipango, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Jamal Kassim Ali kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa na NSSF wakati wa Maonesho ya Wiki ya Huduma za Fedha kitaifa katika viwanja vya Mnazi mmoja.
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Masha Mshomba (wa kwanza mstari wa mbele) akiwa katika ufunguzi wa Maonesho ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa, viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi, Afisi ya Rais Fedha na Mipango wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Jamal K. Ali (aliyekaa katikati), akiwa katika picha ya pamoja na Kamishna Uendelezaji wa Sekta ya Fedha kutoka Wizara ya Fedha Dkt. Charles Mwamwaja (kushoto) na Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Fatma Nyangasa na viongozi wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii.
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Masha Mshomba, akiwa katika maadhimisho ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa ambapo alipata fursa ya kutembelea na kupata maelezo katika banda la Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF). Mifuko hiyo ipo katika viwanja vya Mnazi mmoja kutoa elimu kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa kwa wanachama wao.
Mfuko
wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) umesema umefanikiwa kutimiza
malengo yake ya utoaji ya elimu kuhusu hifadhi ya jamii, umuhimu wa
kujiwekea akiba, huduma zinazotolewa kwa njia ya mtandao pamoja na
kueleza fursa za uwekezaji kwa wanachama katika Maadhimisho ya Wiki ya
Huduma za Kifedha Kitaifa yanayoendelea katika Viwanja vya Mnazi Mmoja
jijini Dar es Salaam.
Hayo yamesemwa jijini
humo na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko huo, Masha Mshomba katika ufunguzi wa
maadhimisho hayo ambapo amebainsha kuwa kufanikiwa kutoa elimu ya
umuhimu wa hifadhi ya jamii kwa wateja na watu waliohudhuria katika
banda lao.
" Tumetimiza malengo yetu ya kutoa
elimu kwa wateja tumewaeleza wateja na wanachama umuhimu wa hifadhi ya
jamii inavyomsaidia mtu anapostaafu au anapokosa uwezo wa kufanya kazi.
Mkurugenzi
huyo amesema wametoa elimu ya umuhimu wa kuweka akiba kwa wanachama na
wateja unavyoweza kuwasaidia siku za baadaye hasahasa wanaposhindwa
kufanya, kustaafu na majanga.
Amesisitiza kuwa
mfuko huo si watu waliopo katika sekta rasmi hivyo hata watu wasio
kwenye sekta hiyo wana fursa kujiunga na kuchangia kwani manufaa yake ni
makubwa.
Amefafanua kuwa wateja na wanachama
wamepewa elimu ya kuwekeza katika maeneo mengine ikiwemo fursa ya
kuwekeza katika hatifungani hivyo wameelezwa kuchangamkia fursa hiyo.
Akifungua maadhimisho hayo
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango, Jamal Kassim Ali
amesema Serikali imepanga kutumia fedha kwenye mitaji ya wajasiriamali
wadogowadogo ambao wanatoa huduma za kifedha kwenye Mpango wa Maendeleo
ya sekta ya Fedha hapa nchini.
Waziri
huyo amaesema elimu ijikite kwenye huduma za Fedha ili waweze kukuza
kipato cha mtu mmojamoja na kuongeza mapato kwa taifa hivyo ni vyema
kujipima ipasavyo ili kuongeza ufanisi kwenye huduma za kifedha hapa
nchini.
Maadhimisho ya Wiki ya Huduma za Kifedha Kitaifa yameanza Novemba 8 na yanatarajiwa kuhitimishwa Novemba 14 mwaka huu.
No comments:
Post a Comment