Waziri wa Viwanda na Biashara Prof. Kitila Mkumbo akizungumza na waandishi wa habari (hawamo pichani,) juu ya Kongamano la Biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na Uingereza litakalofanyika jijini Dar es Salaam.Hussein Ndubikile, Dar es Salaam.
Balozi wa Uingereza nchini Tanzania David William Concar akizungumza na waandishi wa habari kuhusu Kongamano hilo baina ya Uingereza na Tanzania litakalofanyika Novemba 16 mwaka huu jijini Dar es Salaam.
Waziri
Mkuu Kassim Majaliwa anatarajia kufungua Kongamano la Biashara kati ya
Tanzania na Uingereza litakalofanyika Novemba 16 mwaka huu katika Kituo
cha Kimataifa cha Mikutano wa Mwalimu Julius Nyerere, Dar es Salaam.
Hayo
yamesemwa leo jijini humo na Waziri wa Viwanda na Biashara Profesa
Kitila Mkumbo wakati akizungumza na wanahabari kuhusu kongamano hilo.
Amesema
kuwa kongamano hilo litafunguliwa na Waziri Mkuu Majaliwa na
kuhudhuriwa na Mjumbe Maalumu wa Uingereza wa Masuala ya Biashara wa
Waziri Mkuu wa nchi hiyo, Lord Walney na kwamba washiriki takribani 200
kutoka Sekta Binafsi za nchi mbili watahudhuria huku wengine watashiriki
kwa njia ya mtandao.
" Kongamano hili
limeandaliwa kwa namna ya kipekee ili kuongeza tija ya matokeo tarajiwa
ambapo limegawanyika katika makundi matatu yatakayofanya mijadala kwa
wakati mmoja, yaani majadiliano kati ya Serikali ya Tanzania na ya
Uingereza, baina ya sekta binafsi ya nchi hizo mbili pamoja na mdahalo
kati ya Serikali na sekta hiyo," amesema Waziri Profesa Mkumbo.
Amebainisha
kuwa kauli mbiu ya kongamano hilo ni Kuimarisha Ustawi Endelevu wa
Kiuchumi kati ya Tanzania na Uingereza, hivyo litatoa fursa kwa
washiriki kujadiliana kwa kina na kubaini fursa mpya za ushirikiano
baina nchi hizo mbili.
Amesisitiza kuwa kupitia
majadilainao hayo pande zote mbili zitaweza kupanua zaidi wigo wa
ushirikiano katika maeneo ya biashara na uwekezaji hususan sekta za
nishati, madini, miundombinu, kilimo, uchumi wa bluu na utalii.
Ameongeza
kuwa kwa mujibu wa takwimu za Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC) Nchi ya
Uingereza ni ya pili kwa uwekezaji hapa nchini ikiwa na miradi 945
yenye thamani ya Dola za Marekani 5.42 bilioni na kutoa ajira 275,384.
Pia
amesema kuwa takwimu za Serikali ya Uingereza jumla ya thamani ya
biashara baina ya nchi hizi mbili kwa mwaka 2021 ilikuwa pauni za
Uingereza 156 milioni, huku nchi hiyo ikiuza hapa nchini bidhaa zenye
thamani ya Pauni 127 milioni, na Tanzania ikiuza Uingereza bidhaa zenye
thamani ya Pauni milioni 29.
Kwa upande wake,
Balozi wa Uingereza nchini, David Concar amesema kongamano lina umuhimu
kwa nchi zote kwani linakwenda kufungua fursa mpya za uwekezaji
zilizopo.
Balozi huyo amesema katika kongamano
hilo kutakuwa majadiliano baina ya Serikali ya Tanzania na UIngereza,
sekta binafsi pamoja wawkilishi wa makampuni hivyo fursa mbalimbali za
uwekezaji zitajadiliwa.
No comments:
Post a Comment