HABARI MSETO (HEADER)


January 29, 2022

NANI KUMRITHI MAALIM SEIF LEO

 Chama cha ACT Wazalendo leo Januari 29, 2022 kinafanya Mkutano Mkuu Maalum kwa kuchagua viongozi  watakaokiongoza chama hicho.

Moja ya nafasi hizo ni Mwenyekiti wa chama Taifa iliyoachwa wazi na Marehemu Maalim Seif Sharif Hamad aliyefariki dunia Februari 17, 2021.

Nafasi nyingine ni Makamu Mwenyekiti pamoja na nafasi moja ya Halmashauri Kuu ya Taifa.

Mgeni rasmi wa Mkutano huo ni Kiongozi wa chama kikuu cha Upinzani nchini Zimbabwe cha Citizen Coalition for Change (CCC), Ndugu Nelson Chamisa.

 

Mwenyekiti wa Ngome wa Vijana Abdul Nondo, akiwa katika ukumbi wa mkutano Mkuu Maalum wa Chama cha ACT Wazalendo leo Januari 29, 2022 jijini Dar es Salaam.

Baadhi ya wajumbe wa mkutano Mkuu Maalum.

Baadhi ya wajumbe wa mkutano Mkuu Maalum wa Chama cha ACT Wazalendo wakiwa ukumbini.

 Baadhi ya wajumbe wakisoma wasifu wa wagombea.

 Baadhi ya wajumbe wa mkutano Mkuu Maalum wa Chama cha ACT Wazalendo wakiwa ukumbini.

No comments:

Post a Comment

Pages