HABARI MSETO (HEADER)


 


Breaking

July 26, 2022

Serikali yaviasa Vyuo Vikuu kushirikiana na Vyuo vya Nje kuendelea kuboresha Elimu ya Juu

Na Hussein Ndubikile, Dar es Salaam

Serikali imeviasa Vyuo Vikuu Nchini viingie ushirikiano na Vyuo Vikuu vya nje ili kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali kuboresha sekta ya elimu iendane na mahitaji ya soko la ajira la ndani na nje.

Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu a Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknoloja Dkt. Francis Michael katika Kilele cha Maonesho ya 17 ya Elimu ya Juu, Sayansi na Teknolojia yaliyoandaliwa na Tume ya Vyuo Vikuu Nchini (TCU)  katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam.

Amesema kuwa vyuo vikishirikiana na vyuo vya nje vitasaidia kukuza sekta ya elimu kwa kubadilshana uzoefu wa jinsi kuviendesha hali itakayosababisha vyuo vya nje kuwekeza hapa nchini.

" Naviasa vyuo vya ndani viingie link na vyuo vya nje kuendelea kuboresha sekta ya elimu hata vya nje vije kuwekeza Tanzania," amesema Dkt. Michael.

Amebainisha kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inaendelea kufanya kwenye ya sekta ya elimu ikiwemo kuimarisha udhibiti ubora wa vyuo vikuu, kuhakikisha programu za masomo zina wahadhiri wenye sifa na miundombinu, kutenga fedha za udhibiti ubora pamoja na kuongeza ufadhili wa fedha za mikopo.

Amesisitiza kuwa katika kuendelea kuboresha sekta ya elimu ikiwemo kutenga Sh Bilioni 6.4 za udhibiti ubora wa mifumo na mitaala pamoja na kuongeza fedha za mikopo Sh Bilioni 573.

Ametoa wito kwa vyuo vikuu vinavyodahili wanafunzi kufuata sheria na utaratibu za udahaili ili kuepuka kuwasababishia hasara waombaji wa nafasi za masomo na kwamba vitakavyokiuka Serikali itavichukulia hatua za kisheria.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa TCU, Profesa Penina Mlama amesema kuwa tume hiyo itaendelea kuboresha mifumo ya udhibiti ubora wa ndani na kuishukuru wizara hiyo kwa ushauri unaoisaidia kutekeleza majukumu yake kikamilifu.

Amewashukuru wananchi na washiriki kwa kushiriki maonesho hayo na kuongeza kuwa yametoa fursa kwa vyuo vikuu na taasisi shiriki kujitangaza na kuimarisha mahusiano.

Nae Katibu Mtendaji wa tume hiyo, Profesa Chares Kihampa amesema kuwa jumla ya taasisi 75 zimeshiriki maonesho ya mwaka hivyo wataendelea kushirikiana na vyuo vikuu ili kutimiza malengo ya Serikali ya kutoa elimu.

Makamu Mwenyekiti wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA), ambaye pia ni Mwakilishi wa Washiriki, Raphael Chibunda ameipongeza TCU kwa kuendelea kuanadaa maonesho kwani wamefaidika kuongeza idadi ya waombaji kutoka 6,000 kufikia 13,000.

Ameishukuru wizara kwa kuweka msukumo kwenye maonesho pamoja na kuishauri TCU kuvialika vyuo vya Bara la Afrika kuja kushiriki.    


 

No comments:

Post a Comment

Pages